MICHONGO KAMILI

Thursday, 25 September 2014

TUNAOMBA RADHI SAANA KWA WASOMAJ WETU  KWA KUWA OFFLINE KWA KIPINDI CHA MIEZI MIWILI NA WEEKI MBILI....TUMERUDI TENA NA SASA TUNAWAAHIDI KUWAPA VILE VITU ROHO INAPENDA.....WELCOME BACK

SOON UTAUSIKIA MZGO MPYA KUTOKA KWA MAVOKO UNAITWA PACHA WANGU

....JAMAA  ANATISHA  NA DONDOO ZINASEMA MZIGO WA  KIDEO UNAKARIBIA KUACHIWA SOON,,,,,STAY TUNNNNNED!!   HAAAPAHAAPAA NTAACHI   KIDEO PAMOJA NA AUDIO YAKE

Friday, 18 July 2014

TARATIIBU NENO "UGAIDI" LINAANZA KUTAWALA VYOMBO VYA HABARI VYA AFRICA MASHARIKI NA AMANI INATINGISHIKA.

Mmoja wa watu wanaosadikika watuhumiwa wa matukio ya ugaidi nchini Kenya,Jihad Gaibon Swaleh, amefikishwa mahakamani nchini Tanzania.
Mshukiwa huyo amesomewa mashtaka ya kufadhili vitendo vya kigaidi nchini Kenya.




Pamoja naye watuhumiwa wengine 16 ambao wanadaiwa kuendesha vitendo vya kigaidi nchini Tanzania pia wamefikishwa mahakamani hii leo wakikabiliwa na tuhuma za kula njama ya kutenda makosa ya kigaidi nchini Tanzania.
Washtakiwa wote 17 wamerejeshwa rumande baada ya kusomewa mashtaka ya vitendo vya kigadi nchini Tanzania pamoja na nchi jirani ya Kenya.
Upande wa mashtaka ukiongozwa na mwendesha mashtaka ambaye ni wakili wa serikali mwandamizi Prosper Mwangamila ulidai mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, kuwa kwa kutumia mtandao wa facebook aliweza kushawishi watu wengine kuwasiliana kwa lengo la kutafuta vifaa vya kulipua mabomu nchini Kenya na kusababisha majerahi, hofu na Vifo.
Jihand Gaibon Swaleh ambaye amesomewa mashtaka mawili hakuruhusiwa kukiri wala kukana mashitaka yanayomkabili kutokana na kwamba mashitaka hayo yanaangukia katika makosa ya ugaidi ambayo kwa mujibu wa sheria nchini Tanzania mahakama ya Hakimu Mkazi haina mamlaka ya kuendesha kesi za namna hiyo.
Katika kesi ya awali kutajwa mahakamani hapo washtakiwa wengine 16 walisomewa mashtaka mawili ikiwemo kula njama kutenda kosa pamoja na kushawishi wenzao kushiriki katika vitendo vya kigaidi katika sehemu mbali mbali nchini Tanzania.
Ni makosa ambayo wanadaiwa kutenda kati ya Januari mwaka 2013 na Juni 2014 katika maeneo tofauti Tanzania.
Katika kesi zote mbili dhidi ya washtakiwa hao Upande wa mashtaka uliiambia mahakama iliyokuwa chini ya hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo bi Hellen Riwa kuwa upelelezi bado unaendelea na hivyo kuiomba mahakama kuahirisha kesi hizo hadi mwishoni mwa mwezi huu wa Julai.
Awali mapema asubuhi msemaji wa jeshi la polisi nchini Tanzania Bi Advera John Bulimba aliwealeza waandishi wa habari kuhusu tuhuma dhidi ya washtakiwa hao
Hii ni mara ya kwanza kwa kundi kubwa la watuhumiwa kufikishwa mahakamani kwa pamoja wakikabiliwa na tuhuma za makosa ya kigaidi huku mtandao wa kijamii wa facebook nao ukitajwa kuhusika katika kutawanya taarifa za kuwezesha kutenda makosa hayo.
THIS NEWS IS IN RESPECT OF  BBC  SWAHILI…..

Saturday, 7 June 2014

INASEMEKANA ULE UTATA KATI YA MALAWI NA TANZANIA UMEAMKA UPYAAA



RAIS MPYA WA MALAWI AITANGAZIA TANZANIA VITA
RAIS mpya wa Malawi Profesa Peter Mutharika
ametangaza vita na Serikali ya Tanzania,mara tu
baada ya kuapishwa. Akizungumza na Mwandishi
wa Habarimpya.com nchini Malawi baada ya
sherehe za kuapishwa kwake kuhusu kauli yake
aliyoitoa mwaka jana wakati akiajiandaa na
kampeni za uchaguzi mkuu kwamba suala la Ziwa
Nyasa haliwezi kuchukua nafasi katika serikali yake
kwakuwa ziwa ni mali ya Malawi.
"Siwezi kusema chochote kwa sasa kuhusu suala
la Ziwa Nyasa kwa sababu nilisha toa msimamo
wangu hivyo kilicho baki ni utekelezaji"alisema
Rais Mutharika kwa ufupi.
mapema mwaka jana Mutharika alisema kwamba,
nchi zote mbili yaani Tanzania na Malawi hazina
cha kujadili kuhusu suala la Ziwa Nyasa (Ziwa
Malawi) kwa sababu hilo Ziwa ni mali ya Malawi.
Akiwa katika mkutano wa siasa mjini Chipoka
nchini Malawi August 3 2013 Mutharika alisema
kwamba,"Hakuna haja ya kujadili suala la Ziwa
Malawi kwakuwa ni mali ya Malawi na itaendelea
kuwa mali yetu, tutakapo chukua nchini mwakani
ujinga huu wote utamalizika kwa sababu hivi sasa
Tanzania inajigamba kwa sababu Serikali
inaongozwa na viongozi wajinga"alisema Mutharika
na kuongeza:.
"Nitaongeza meli nyingi za uvuvi na usafirishaji
katika ziwa hilo kwa ajili ya kuinua uchumi wa nchi
na ajira kwa vijana wa Malawi, hili litawezekana
kwa sababu Tanzania haina hata inchi moja ya
umiliki wa Ziwa hilo".
Wakati wa utawala wa Rais Joyce Banda Serikali
yake likuwa katika mgogoro na Serikali ya
Tanzania kuhusiana na umiliki wa Ziwa hilo, huku
akitangaza kwamba yuko tayari kupigana vita na
Tanzania ili kuilinda Ziwa hilo lenye utajiri mkubwa
wa mafuta.
Hata hivyo Uchunguzi uliofanywa na Mwandishi wa
Habarimpya.com nchini Malawi imebaini kwamba
kati ya mambo yaliyo mpa Mutharika ushindi ni
pamoja na ahadi yake kwa wananchi kuhusu Ziwa
Nyasa.
Malawi na Tanzania tayari zimewasilisha ushahidi
na majibu ya maswali kuhusu umiliki wa maeneo
kwenye Ziwa Nyasa, kwa jopo la wasuluhishi
linaloongozwa na Rais mstaafu wa Msumbiji
Joachim Chissano.
Wasuluhishi hao walizitaka Malawi na Tanzania
kutoa majibu ya maswali manne muhimu, wakati
wakiwasilisha ushahidi wao kuhusu umiliki wa ziwa
hilo wenye mgogoro. Mgogoro huo uliibuka baada
ya Serikali ya Malawi bila kushauriana na Tanzania
kutoa leseni kwa kampuni mbili za kigeni, kutafuta
mafuta katika eneo la ziwa ambalo linamilikiwa na tanzania Viongozi wa juu wa usalama wa Taifa wamewaomba wanaichi wanaendelea kufanya mazoezi binafsi hata ndani ya vyumba vyao kwaajili ya Kupambana na nduli Prof Mutharika.
Pushapu zinashauriwa zaid kwa ajili ya kuongeza pumzi..

Kuna wasiwas vijana wa vyuo kikuu kupewa kipaumbele zaid kwa ajil ya kutetea nchi yao. Hivyo take your private time to prepare for the war.

HUO NDO MCHONGO WA LEO

Saturday, 26 April 2014

SHEREHE ZA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR ZAFANA.




Sherehe za muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilizo fanyika katika uwanja wa zamani wa taifa zimefana sana kwa halaiki na maonyesho ya kijeshi yaliyofanywa kuanzia asubuhi hadi mchana huku mgeni rasmi akiwa raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania, sherehe hizo zimefanyika huku mwenyekiti wa bunge maalum la katiba akiwa ameahirisha shughuri za bunge hilo ili kupisha bunge la kujadili bajet liendelee na shughuli hiyo hadi mwezi wa nane ndio bunge maalum la katiba litaendelea.

Tuesday, 22 April 2014

HATIMAYA MOYESA ATUPIWA VIRAGO

 

Mkufunzi mkuu na meneja wa klabu ya Manchester United David Moyes ametimuliwa.

David Moyes amefutwa kazi baada ya kushikilia usukuni wa klabu hiyo kwa miezi kumi tu.

Moyes, mwenye umri wa miaka 50, aliteuliwa na Ferguson kumrithi alipostaafu mwaka jana baada ya kuwa na klabu hiyo kwa miaka 26.

Taarifa kutoka kwa klabu hiyo imemshukuru Moyes kwa bidii, uaminifu na hekima aliyoonyesha kocha huyo akiwa mkufunzi wa Manchester United.

Moyes alichukuwa usukani wa kuifunza Manchester United mwaka uliopita baada ya aliyekuwa kocha wa siku nyingi Sir. Alex Ferguson kustaafu.

Huku zikiwa zimesalia mechi nne pekee msimu wa ligi kukamilika Mancheseter united inashikilia nafasi ya saba kwenye jedwali la msimamo wa ligi hiyo alama ishirini na tatu nyuma ya viongozi Liverpool.

Klabu hiyo imeshindwa kufuzu kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa ulaya kwa mara ya kwanza katika kipindi cha takriban miaka ishirini.

NI KIJANA MWENYE UMRI USIO ZIDI MIAKA 25 ALIYE SOMA ALFAROUQ SEMINARY AKAENDA LIDA BOYS ILIYOPO LINDI NA SASA YUPO CHUO FLANI FLANI HIVI AKIWA NA KIPAJI CHA AJABUUUU ALIANZIA KUPAZA SAUTI CHINI YA MITI ALIPO KUWA LIDA BOYS LAKINI ALIPO FIKA CHUO ALIKUTANA NA PRODUCER AITWAE CHRISS NA AKAMPA NAFASI YA KUPAZA SAUTI MBELE YA KIPAZA NA HII NGOMA HAPO CHINI NDICHO KILICHOJIRI.............PERFECT FOR BEGGINER! NAIDEDIKET HII KWA WAPENZI WA BLOG HII .....I MISS YOU SO MUCH



Sunday, 13 April 2014

ALAZWE MAALI PEMA PEPONI REJENDARI MAALIM GURUMO




inna lilah wainna ilaih rajiun...Ni mzee wa siku nyingi sana kwenye
muziki Tanzania ambae aliwahi
kuingia kwenye vichwa vya habari
mara nyingi hasa kutokana na
kuugua kwake kuliko mfanya asitaafu
kabla ya kuzawadiwa gari na
mwanamziki wa kizazi kipya
“Nasibu” au Diamond
Taarifa zilizothibitishwa na hospitali
ya Taifa Muhimbili  zimesema Mzee huyu
amefariki dunia akiwa hospitalini
hapo leo April 13 2014 saa nane
mchana baada ya kupelekwa  jana
asubuhi na kulazwa kwenye wodi
namba 6 ya Mwaisela kutokana na
kuzidiwa.
Tayari mwili wake umepelekwa
kwenye chumba cha kuhifadhia maiti
msiba upo nyumbani kwa marehemu Tabata makuburi
na mimbango ya mazishi itafanyika hapo.
Blog hii inatoa pole kwa wafiwa wote na
wapenzi wa muziki mzuri uliokuwa ukifanywa na
mzee wetu Maalim gurumo
MUNGU AILAZE MAHALI PEMA
PEPONI ROHO YA MAREHEMU
MAALIM GURUMO
“AMIN"
Breaking News
Loading...

Search This Blog

LIKE PAGE ZETU ZA FACE BOOK

ZINGINE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...