HATIMAYE Shirikisho la 
Soka Duniani, FIFA limemuidhinisha mshambuliaji nyota wa kimataifa wa 
Uganda, Emmanuel Okwi kuichezea klabu ya Yanga. Kwa mujibu maelezo wa 
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka nchini, TFF, Celesine Mwesigwa 
amethibitisha kuwa tayari wameshapokea barua kutoka FIFA ikiwahabalisha 
kuwa mchezaji huyo ni halali kukipiga Yanga. Mwesingwa amesema suala 
Okwi tayari limeshamalizika ila hawezi kulizungumzia zaidi kwasababu 
watatuma taarifa kwa vyombo vya habari kwa ufafanuzi zaidi. Januari 22 
mwaka huu ikiwa ni siku mbili tu kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa
 Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Kamati ya Sheria na Hadhi za 
Wachezaji ya TFF ilisimamisha usajili wa Okwi kuitumikia Yanga ili 
kwanza upatikane ufafanuzi kutoka FIFA juu ya uhalali wake kucheza timu 
hiyo. Kamati hiyo ilifikia iliamua hivyo kwasababu ya mgogoro wa 
mchezaji huyo na klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia ambapo kulikuwa na 
taarifa kuwa alipewa kibali cha muda kuichezea SC Villa ya nchini kwao 
ili kulinda kiwango chake.Friday, 21 February 2014
OKWI RUKSA KUCHEZA YANGA - FIFA.
HATIMAYE Shirikisho la 
Soka Duniani, FIFA limemuidhinisha mshambuliaji nyota wa kimataifa wa 
Uganda, Emmanuel Okwi kuichezea klabu ya Yanga. Kwa mujibu maelezo wa 
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka nchini, TFF, Celesine Mwesigwa 
amethibitisha kuwa tayari wameshapokea barua kutoka FIFA ikiwahabalisha 
kuwa mchezaji huyo ni halali kukipiga Yanga. Mwesingwa amesema suala 
Okwi tayari limeshamalizika ila hawezi kulizungumzia zaidi kwasababu 
watatuma taarifa kwa vyombo vya habari kwa ufafanuzi zaidi. Januari 22 
mwaka huu ikiwa ni siku mbili tu kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa
 Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Kamati ya Sheria na Hadhi za 
Wachezaji ya TFF ilisimamisha usajili wa Okwi kuitumikia Yanga ili 
kwanza upatikane ufafanuzi kutoka FIFA juu ya uhalali wake kucheza timu 
hiyo. Kamati hiyo ilifikia iliamua hivyo kwasababu ya mgogoro wa 
mchezaji huyo na klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia ambapo kulikuwa na 
taarifa kuwa alipewa kibali cha muda kuichezea SC Villa ya nchini kwao 
ili kulinda kiwango chake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Breaking News
  Loading...
No comments:
Post a Comment
0653830825