MICHONGO KAMILI

Wednesday, 19 February 2014

"HIVI SASA NI WAKATI WA KUTENGENEZA IMAGE YA JERUSALEM PEKEE".................... ASEMA JACOB STEVEN

YULE MKALI WA SHKAMOO MZEE NA NYINGINE NYIIINGI YAANI "JB" JACOB STEVENANAKUJA NA CHUMA KINGINE "WAGENI WANGU"

TRAILLER YA WAGENI WANGU

Utakapozungumzia watengenezaji wazuri wa
filamu za Kitanzania huwezi kuacha kuwataja Jerusalem
Film ambayo kampuni hii ipo chini yake Bonge la Bwana “JACOB STEVEN” ambaye pia
katika waigizaji wanaofanya poa sana
hivi sasa katika soko la filamu ndani na nje ya nchi pia huwezi kuacha

kumuorodhesha huyu jamaa.

JB KATIKA POUZI
Juzi kati tulipata fursa ya kuzungumza
nae na tukataka kufahamu mengi sana kutoka kwake
lakini pia kutokea Jerusalem Film akiwa kama mzungumzaji mkuu wa Kampuni hiyo. Na kitu cha mwanzo
kabisa tulichotaka kufahamu ni kuhusiana na suala zima la Jerusalem kutoa
filamu ambazo JB hatujamuona humo ndani hata scene moja, jambo ambalo
limewaumiza vichwa mashabiki wake wengi katika filamu iliyokwenda kwa jina la
BADO NATAFUTA.
alikuwa na haya yakusema;
“Yeah ni kweli, ila lengo la kufanya
hivyo ni kutaka kutengeneza image ya kampuni ya Jerusalem
Film na si lazima ya JB, kwa maana ya kuwa watu wawe na hamu ya kutazama filamu
za Jerusalem. Na
huo naweza nikasema ndiyo mpango wa hivi sasa kwa maana ya kuwa kutakuwa na
filamu za aina mbili ambazo nitakuwa sishiriki na zile ambazo nitakuwa
nashiriki”.
OFFICIAL COVER YA MOVIE AMBAYO IMEFANYA POA SANA 2013 "BADO NATAFUTA"
Lakini jambo jengine ambalo JB
alilizungumzia ni kwamba anawashukuru sana mashabiki wake kwani filamu hiyo ya
BADO NATAFUTA imekuwa filamu ambayo imefanya vizuri sana mwaka jana.Ila bado
tukawa na maswali kwa JB kuwa kwanini ameamua kuhamia katika kutengeneza image

ya Kampuni tu na si JB kama JB?
 
Bi Staa kama anavyojulikana na wengi....
“Hapana, ila unajua jambo muhimu ambalo
tumelilenga hapo ni kuwafanya mashabiki wakishakuwa na imani na Jerusalem ijapo
kuwa JB hayumo ndani ya filamu hiyo itasaidia sana pale ambapo nitakuwa siigizi
tena kutokana na sababu mbalimbali huwenda nimeamua kupumzika, au kwa sababu
nyengine yeyote ile. Hivyo watu bado watakuwa na imani na vitu vinavyozalishwa
na Jerusalem.”
GABO AKIWA KAZINI
Na jambo jengine ni kuhusiana na
mipangilio ya Jerusalem kwa mwaka huu 2014, maana tayari ni mwezi wa pili huu
hivi sasa tunaelekea na hatujaona wala kusikia kazi yeyote mpya kutokea kwako.
Suala ambalo alinieleza kuwa wapo vyumbani wakikamilisha mapishi ya kazi mpya nyiingi
tu ambazo soon zitakuwa sokoni.
GABO AKIWA KAZINI ALIYEKUWA MAIN CHARACTER NDANI YA BADO NATAFUTA
“Kwa filamu ambzo mimi sishiriki mwaka
huu tutakuwa na filamu itakayoitwa WAGENI WANGU ambayo ameshiriki Bi
Hindu,Mhogo Mchungu,Bi Star, na  mzee
mwingine wa Mombasa ambayo hii itatoka recently, halafu tutakuwa na POLICE LOCK
UP ambayo atakuwepo Ben Kinyaiya,Brigit (ambaye ameigiza kama Regina) na Adam
Kuambiana, then tutakuwa na filamu nyingine inaitwa  CHA USIKU ambayo wameshiriki Mayasa Mrisho,
Hemed Suleiman,Cathy Rupia, Shamsa Ford, Brigity na Baba wa Hisia “Haji Adam.
Ila kwa upande wa movie ambazo nashiriki ya kwanza kabisa itakuwa ni HUKUMU YA
NDOA YANGU ambayo nimecheza na muigizaji wa siku nyingi sana Chiki Mchoma,
Mayasa Mrisho, Shamsa Ford, Bi Mwenda, Q Chief, Brigity na Will Sanga. Ambapo
nafikiri movie hii itatoka mwezi wa tatu ama nne”
 
Katika malengo mazuri kabisa ya JB kwa
kutengeneza image ya kampuni yake ni pamoja na suala zima la kuwapa nafasi  au kuwafungulia milango waigizaji mbalimbali
wadogo ili kuwapa nafasi na kuwa waigizaji wakubwa na waigizaji wapende kuigiza
Jerusalem
either JB yupo ama hayupo. Sasa suali langu lilikuja likiuliza kuwa je ni
kuibua  vipaji au vipi maana kama ni kuibua vipaji hatujaona katika mfululizo huo
alionitajia jina ambalo ni jipya katika masikio yetu lakini pia hata katika

movie ya Bado Natafuta halikadhalika.
GABO KATIKA POUZI
“Swali zuri sana, Jerualem haibui vipaji
ila ni inaendeleza vipaji maana kuibua vipaji ni risk. Maana wapo waigizaji
waliokwisha anza kuigiza na wana vipaji, hivyo sera yetu ni kuwapa nafasi

waigizaji hao na kuwafanya wawe waigizaji wakubwa kwa kuwapa movie nyingi.”
JB AKIFURAHIA KAZI NZURI WALIYOIFANYA ZANZIBAR BAADA YA KUTWAA KITU HICHO (KOMBE0
Baada ya maongezi mengi sana na Bonge la Bwana “JB” kupitia 92.5 Hits
fm radio ikishirikiana na Www.ridhiwanshariff.blogspot.com,
kabla ya kumpa nafasi ya kuzungumza na fans wake ikanibidi na mie nimpatie

hongera yake kwa movie ya BADO NATAFUTA kwani hata mie imenivutia.
JB KATIKA POUZI YA PICHA NA JEZI YA TANZANIA
“Thanks bro, Nawaahidi kuwa movie ambazo
tumezitengeneza mwaka huu 2014 watazipenda sana maana waigizaji hawa waliocheza nimekaa
nao kwa muda mrefu tumefundishana, tumeelekezana na kila mmoja ameonesha ana
uwezo mkubwa. Hivyo nawaahidi kwamba hata movie ambazo sitashiriki watazipenda
sana kama ambazo nimeshiriki na mfano wameshaanza kuona kwa BADO NATAFUTA ni
filamu ambayo imefanya vizuri sana na hata zile ambazo nimeshiriki zingine

hazikupendwa sana kama hii ambayo sijashiriki”.


KUPITIA HAPA
HAPA Www.Michongokamili.com UTAWEZA KUSIKIA INTERVIEW YA
JACOB STEVEN NA RIDHIONE SHARIF WA ZANZIBAR
JACOB NA IRENE  KAZINI

Thursday, 9 January 2014

DIAMOND FT DAVIDO - MY NUMBER ONE REMIX

NI DIAMOND KWA MARA NYINGINE  AKIJA NA NGORORO 
AKIWA KAMSHIRIKISHA DAVIDO !!!!!

 
ACHA MOVIE LIENDELEEEEE!!!!!!!

Monday, 30 December 2013

NEY WA MITEGO NI FREEMASSON?

 FREEMASSON NA NEY WA MITEGO !!!!!!!
Blog hii kwa mara ya kwanza imeamua kukuletea jambo ambalo limekuwa gumzo sana midomoni mwa watu.......ni kuhusu uwepo wa dini ya kishetani iitwayo freemasson,inasemekana kuwa  uwepo wa dini hii ume kuwa ni wa kificho sana ....lakini kwa ushahidi mbakli mbali inaonyesha kuwa dini hiyo ipo na ina endesha shughuri zake ulimwengu mzima... ushahidi mmoja wapo ni uwepo wa freemasson hall mjini dar es salaam maeneo ya posta ambalo ni hili hapa chini kama lionekanavyo kwenye picha..
inasemekana dini hiyo imekuwa ikiwashawishi wasanii wakubwa ambao ni kioo cha jamii ili kujiunga na dini hiyo ili kuwa poteza mashabiki wa msanii hao, baadhi ya wasanii wamewa wakitajwa kujihusisha na dini hiyo majina kama DIAMOND PLATNUMZ  na  NEY WA MITEGO yamekuwa yakitamkwa sana mitaani huku yakihusishwa sana na dini hiyo huku sababu kubwa ikiwa ni matendo yao,maneno,skendo,na alama tofauti tofauti ambazo wamekuwa wakizionyesha kwenye mausha yao ya muziki,,,,,,,je   kuna  ukweli  wowote? kwa leo  tutaanza  na ushahidi kadhaa uliokusanywa na blog hii kuhusu msanii ney wa mitego....
Ney wa mitego ametokea kuwa nsanii aliye teka sana soko la muziki wa hip hop hivi karibuni lakini amekuwa akipunguza mashabiki kutokana na skendo mbalimbali kama hii inayo onekana hapa chini.

Tukiachana na skendo hizo bado kume kuwa na alama mbali mbali ambazo msdanii huyo amekuw akizionyesha kwenye video zake huku aki tamka maneno ambayo yana mtambulisha yeye kama rafiki wa dini hiyo kwa mfano kwenye nyimbo yake maaru iitwayo "NASEMA NAO" alimetoa sentensi kadhaa ambazo zina dhihirisha uhusika wake katika dini hi yo kwa mfano aliposema "unataka kwenda mbinguni huwezi fika bila mii" swali ni kwamba  yeye ni nani???? pia  mstari mwingine ni ule usemao "mimi ndo rafiki wa lucifer !! utanieleza nini " yeye ni rafiki wa LUCIFER  na lucifer ni mungu wa dini hiyo kama anavyo onekana hapa chini
pia amekuwa akionyesha alama mbali mbali ambazo ni alam,a za dini hiyo kama inavyoonekana hapa chini
hakuishia hapo pia katika video yake iitwayo "NASEMA NAO" ameonyesha alama hizo mara nyingi zaidi na kwakukusudia kabisa kwa mfano katika picha zifuatazo

je hii ni bahati mbaya? au ni swaga kama wasemavyo vijana wa mjini ambao wamekumbwa na mkumbo huo wa kuiga matendo ya wasanii wakubwa huku wakiita swaga!!!!!!! tuendelee!!

je na hii ni bahati mbaya? au bado ni swaga? sijui!!

  hatuhitaji kutumia miwani kuona alama hizi !!
huu ni ushahidi tu uliokusanywa na blog hii na halazimishwi mtu kukubaliana na ushahidi huu....
mhhhhhhhhhhhhhhhhh!!!!!!!
mwishoni mwa nyimbo hiyo anasema hivi  "I represent my hood" lakini badala ya kuonyeshwa manzese anaonyeshwa akiwa na watu kadhaa ambao wamevaa mavazi ya kufunika ambayo inaaminika kuwa hutumika katika ibada za freemasson je? ana represent manzese au makundi ya watu hao? kilichoonyeshwa ni hiki!!!

haya ni mambo kadhaa tu anayo yafanya msanii huyun  nakufanya wengi waamini juu ya uhusika wake kwa dini hiyo ya FREEMASSON   Lakini vipi kuhusu DIAMOND?
Acha blog hii ikusanywe kwanza kisha itarudi jamvini kuwapasha yaliyomo!!!   ALLEVIDEH!

Tuesday, 3 December 2013

Viongozi wa jumuiya ya afrika mashariki waliokutana mjini Kampla Uganda wametia saini sheria ya makubaliano ya kuwa na sarafu ya pamoja.



Kutiwa saini kwa makubaliano hayo ni hatua muhimu ya kukuza mshikamano wa jumuiya hiyo yenye nchi tano.
Makubaliano hayo ya kisheria yalitiwa saini na viongozi wote watano wa jumuiya ya afrika mashariki kwenye kongamano la 15 lenye maudhui ya kuwa na sarafu moja.
Akizungumza kwenye kongamano hilo katibu mkuu wa jumuiya ya Afrika mashariki bwana Richard Sezibera anasema kubuniwa kwa mkataba wa kuwa na sarafu moja ni hatua muhimu ya mshikamano haswa baada ya kuwa na soko la pamoja na umoja wa forodhani ambazo zinasaidia usafirishaji wa bidhaa na mitaji.
"Eneo letu linapiga hatua kubwa ya mshikamano haswa baada ya kutiwa saini kwa makubaliano ya kuwa na sarafu moja. Umoja huu wa sarafu unaiweka jumuiya yetu kwenye awamu nyingine na ni hatua muhimu. Kutiwa saini kwa makubaliano Haya pia ni mwamko mpya wa mshikamanno wa kifedha."
Kutiwa saini kwa sheria hii ya sarafu moja kunatoa nafasi kwa nchi wanachama kuanza kuondoa sarafu zao za ndani ya nchi ili baadaye kuanza kutumia sarafu ya pamoja kote kwenye jumuiya ya afrika mashariki.
Mwenyekiti mpya wa jumuiya hiyo ambaye ni Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta anaiona hii kama hatua muhimu ambayo itavutia zaidi wawekezaji kwenye eneo la afrika mashariki.
"Wafanyi biashara watapata Uhuru zaidi wakufanya shughuli zao huku nao wawekeaji wakiongezeka wakipata fursa bora ya kuja kwenye kanda hii. Tukiwa na manufaa kama hayo bila shaka uwekezaji utaongezeka na kuboresha uchumi wetu"
Chini yasheria hii nchi wanachama wa EAC wanatakiwa kuwasilisha sera zao za kubadilisha fedha kwenye benki kuu ya afrika mashariki itakayobuniwa, hii ikiwa ni hatua za kuelekea kuwa na sarafu ya pamoja.
Wajibu wa benki hiyo kuu ya afrika mashariki itakuwa ni kuthibiti dhamani ya sarafu moja na pia kusimamia maswala yote ya kifedha kwenye kanda.
Lakini ingawa viongozi wa afrika mashariki wanaisifu hatua hii ya sarafu moja na kuitaja kuwa yenye manufaa kwa mshikamano, wataalam wanahoji kwamba bado kuna maswala muhimu kuliko kuwa na umoja wa sarafu kama vile biashara baina ya nchi wanachama.
Bwana Louis Kasekende ni naibu gavana wa benki kuu ya Uganda.
"Sitaki tuzingatie kupita kiasi kuwa na sarafu ya pamoja. Lazima pia tuzingatie mambo ambayo tungependa kufanikishsa Kama vile maswala ya maendeleo ya kiuchumi. Tunahitaji kufanya biashara zaidi kwa kuuza bidhaa na huduma miongoni mwetu."
Lakini Gavana wa benki kuu ya Tanzania Profesa Benno Ndulu ana maoni tofauti.
"Tutakuwa tu na sarafi moja kwa hiyo inarahisisha sana biashara na inarahisisha pia kuwa na soko moja kubwa"
Tayari jumuiya ya afrika mashriki imefanikiwa kubuni soko la pamoja na umoja wa forodha hali ambayo imeimarisha biashara kufuatia kuondolewa kwa vikwazo vya barabarani na pia mipakani.
Nchi zote tano zina zaidi ya watu million 135 na kwa pamoja zina pato la jumla la dola bilioni 85.

Mkataba huu wa sarafu moja uliotiwa saini leo utatekelezwa ndani ya miaka kumi na hapo ndipo jumuiya ya afrika mashariki itaanza kutumia pesa moja tu.

NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI KUTUMIA SARAFU MOJA BAADA YA MIAKA 10

NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI KUTUMIA SARAFU MOJA BAADA YA MIAKA 10
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6HV-LW830SD6AESsqbWZBWw3W6BPQpPw-32PrjPAUbyNf6DPK3oK_hoIVvFmMoGAGC3AqmK07AtmWT84jKi2UXJmwef71-5rLiV0j3gd5UlyvA4j3vFbMigUV6J971bQagFN5sc_yWg9y/s640/MONETA.jpg
Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) anayeshughulikia Miundombinu,Dk Enos Bukuku akizungumza na waandishi wa habari jijini Kampala leo juu ya hatua zilizofikiwa katika kuweka saini Itifaki ya Sarafu Moja jumamosi wiki kwenye Uwanja wa Kololo nchini Uganda,kushoto ni Mkufunzi na Mwandishi Mkongwe,Jenerali Ulimwengu.

Na Mwandishi Wetu,Kampala

Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jumamosi wiki wameweka saini Itifaki ya Sarafi Moja ikayowezesha matumizi ya Sarafu moja katika nchi hizo.

Matumizi ya Sarafu moja yatachukua muda kutekelezwa  ili kutoa nafasi ya utekelezaji wa michakato mbalimbali ya kuoainisha sera na sheria ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa taasisi kadhaa kabla ya kuanza kutumika Sarafu hiyo inaweza  kuchukua miaka 10.

Akizungumza na waandishi wa habari leo ,Naibu Katibu Mkuu wa EAC anayehusika na Miundombinu,Dk Enos Bukuku amesema utaratibu huo utazifanya nchi wanachama kukubaliana katika mambo ya sera za fedha za Jumuiya hiyo na kuwa na Benki Kuu ya EAC.

Amesema wataalamu katika Sekretariat ya Jumuiya hiyo wamekua wakienda kujifunza mfumo wa utendaji kazi wa Sarafu moja kwenye nchi za Umoja wa Ulaya(EU). 

Saturday, 23 November 2013

GAZETI LA AMANI NI NOMA KWAKUCHIMBA 
Diamond kwa sasa ndiye mwanamuziki aliye matawi ya juu zaidi kuliko yeyote kwenye Bongo Fleva, akisumbua vibaya na kibao chake cha Number One wakati Penny akiingiza mkwanja kupitia utangazaji katika kituo cha Runinga ya Dar es Salaam ‘DTV’.
ISHU YABUMBURUKA!
Sosi wa karibu, ndani ya familia ya Diamond alinyetisha kwamba, Diamond na Penny ni ndugu wa damu lakini jambo hilo limefahamika hivi karibuni na hivyo wanahaha namna ya kuzima aibu hiyo.
Kwa sharti la kutochorwa jina gazetini, sosi huyo alisema: “Ndugu kwenye familia wanagongana. Wanajaribu kufichaficha hili jambo, lakini inashindikana. Unajua kinacholeta shida zaidi ni kwamba Diamond na Penny watakavyokuwa baada ya uamuzi kupitishwa.”
Alisema, pamoja na ukweli huo kugundulika bila shaka kuwa ni ndugu, bado kuna ugumu wa wapenzi hao waliozama kwenye dimbwi la mahaba kisha kuvunja amri ya sita, kuachana na kubaki wakiheshimiana kama kaka na dada.
“Tatizo ni je, Diamond atakubali kumchukulia Penny kama ndugu yake? Kama atakubali na Penny naye atakuwa tayari? Wote kwa pamoja wanaonekana kama wanapingana na jambo hilo,” alisema.
UNDUGU WENYEWE UKOJE?
Akieleza aina ya unasaba wa Diamond na Penny, sosi wetu huyo alisema, bibi mzaa mama wa Diamond na bibi mzaa mama wa Penny, wamezaliwa na mama mmoja.
Hapa anafafanua: “Kwa sababu hiyo sasa, unaweza kuona kuwa, wale ni sawa tu na mtu na kaka yake. Tena wako ndani ya ukoo kabisa, sema hao mabibi, kila mmoja alikuwa na baba yake, walichangia mama tu.
“Familia imejiridhisha kabisa, halafu isitoshe imeonekana kuwa, undugu wa kuchangia mama ndiyo wa uhakika zaidi kuliko wa baba ambao mtu anaweza kubambikwa hata mtoto asiye wake. Kifupi Penny na Diamond ni ndugu. Sema ndiyo hivyo historia za wazazi wao zinashangaza mpaka basi.”
Kwa mujibu wa sosi wetu, majina ya bibi hao wanaounganisha undugu ni Khadija Said Abas (bibi yake Penny) na Tatu Omar (bibi yake Diamond), wote kwa sasa wametangulia mbele ya haki.
“Kinachoshangaza sasa, mama Diamond amefurahi sana na amezidisha mapenzi yake kwa Penny, ndiyo maana hataki kusikia mwanaye anakuwa na mwanamke mwingine zaidi ya Penny.
“Mwenyewe anasema, kwanza undugu siyo wa karibu sana hivyo haina madhara lakini pia anajua Diamond atampenda, kumheshimu na hatamnyanyasa kwa sababu ni sehemu ya damu ya familia yao,” sosi aliendelea kutiririka.
HAPA AMANI, KULE DIAMOND
Amani lilifanya juhudi za kumsaka Diamond katika simu zake zote za mkononi bila mafanikio, likahamia kwenye mitandao ya kijamii, likamnasa ambapo awali mahojiano yalikuwa na kigugumizi lakini baadaye mambo yalikuwa hivi;
AMANI: Mzee vipi, mbona hupatikani kwenye simu zako zote? Kuna jambo nataka kukuuliza bwana mkubwa.
DIAMOND: Niko Nigeria. Vipi, kuna nini tena?
AMANI: Kuna stori fulani... eti ni kweli bibi yake Penny mzaa mama na bibi yako wewe ni ndugu wa damu kwa maana wamezaliwa na mama mmoja?
DIAMOND: Yeah but wamechangia mama, kila mmoja na baba yake.
AMANI: Kwa hiyo Penny ni dada yako kiasili si ndiyo?
DIAMOND: Yap!
AMANI: Duh! Majanga... kwa hiyo unatembea na dada yako wa damu?
DIAMOND: Nilikuwa najua basi kaka?!
AMANI: Kwa hiyo sasa baada ya kugundua hivyo, unaachana naye au?
DIAMOND: Kama nilivyokuambia, niko Nigeria... halafu niko gym sasa hivi, nitakutafuta nikitoka.
AMANI: Sawa, naomba ujibu hili swali la mwisho. Tumesikia kuwa, mama yako anampenda sana Penny, ni kwa sababu amegundua kuwa una undugu naye?
DIAMOND: Ha! Ha! Ha! Nikitoka gym nitakupigia simu tuzungumze vizuri.
Diamond hakufanya hivyo. Hata alivyotafutwa baadaye kwenye mtandao huo, pia hakuonekana kuwa hewani.
PENNY MIKONONI MWA AMANI
Penny alipopatikana juzi Jumanne, kwa njia ya simu alielezwa ilivyo ambapo alisema: “Ni kweli Diamond ni ndugu yangu wa damu. Tumegundua tukiwa tayari tumeshakuwa wapenzi.
“Hakuna jinsi tena, sanasana naona kama mapenzi yetu ndiyo yamezidi kuimarika. Nampenda sana Diamond wangu na sababu hiyo haitoshi kututenganisha maana kama ni makosa tayari yameshatokea.”
MAMA DIAMOND
Kwa upande wake mama Diamond, baada ya kusimuliwa kila kilichofika mezani mwa Amani na kutakiwa kueleza msimamo wake alijibu kwa kifupi: “Ndiyo ni kweli unayosema, lakini kwa sasa nipo huku Kariakoo (Dar), sipo kwenye nafasi nzuri ya kuzungumza. Njoo nyumbani jioni, tuzungumze vizuri.”
Diamond na Penny wamekuwa kwenye penzi lenye kasheshe nyingi kufuatia mwanamuziki huyo kuhusishwa na wanawake wengine akiwemo aliyekuwa mpenzi wake wa zamani, Wema Isaac Sepetu.


MAJANGA REMIX YA DOGO SKIDE

Breaking News
Loading...

Search This Blog

LIKE PAGE ZETU ZA FACE BOOK

ZINGINE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...