MICHONGO KAMILI

Saturday, 26 September 2015

TAMKO LA TAASISI YA KIISLAM (IMAM BUKHARY) JUU YA KAULI ZA EDWARD LOWASSA NA ASKOFU GWAJIMA


Ndugu Wanahabari,

Assalaam Alaykum,

Hivi karibuni Taifa letu limetikiswa na maneno ya hatari yaliyotoka katika vinywa vya watu wawili mashuhuri hapa nchini. Maneno ambayo endapo yatapuuzwa yatasababisha mpasuko mkubwa wa kijamii na pengine maafa, na hatimaye kubomoa misingi imara ya taifa iliyojengwa na waasisi wa Taifa hili. kauli hizo ni zile zilizotolewa na mgombea urais wa CHADEMA Ndugu Edward Lowassa na kiongozi wa Kanisa la ufufuo na uzima, Askofu Josephat Gwajima.

Mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA Ndugu Edward Lowassa amenukuliwa akiwa Kanisani Mkoani Tabora akiwaomba Waumini wenzake wa Madhehebu ya Kilutheri kumuombea sana awe Rais wa Taifa letu kwa hoja kuwa nchi hii haijawahi kupata Rais Mlutheri.

Naye Askofu Josephat Gwajima ambaye ni mshirika wa karibu wa Lowassa amenukuliwa pia akielezea ndoto yake ambayo bado haijatimia ya Kuiona Misikiti ya Tanzania ikigeuzwa kuwa “Sunday Schools” za watoto, pamoja na Masheikh na Maimamu kukimbizana kwenda mbele ya msalaba wa Bwana Yesu Kristo (AS).

Maneno haya ya Ndugu Lowassa na yale ya Askofu Gwajima yakitazamwa kwa idadi ni machache sana, lakini kwa uzito wake ni mabaya tena yenye hatari kubwa kwa umoja wetu wa kitaifa.

Maneno hayo yanaweza kulisambaratisha taifa kwa vile yanaonyesha dhamira mbaya waliyo nayo viongozi hao katika kuibomoa misingi ya Utaifa ya umoja na mshikamano, na badala yake kujenga misingi ya udini katika siasa na utawala.

Kadhalika matamshi hayo yanaonyesha dhamira yao ovu ya kujenga utawala wenye kufuata misingi ya ubaguzi wa kidini endapo watafanikiwa kushika uongozi wa nchi, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa Uislamu unafutika kabisa katika nchi hii.

Ndugu Wanahabari, tujikumbushe kwamba Edward Lowassa anaomba awe Rais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na mchakato wa kumfikisha huko umeratibiwa na Askofu Gwajima. Kila mmoja kati yao ameweka wazi dhamiri yake.

Wakati Ndugu Lowassa amejikita katika fikra za kupandikiza dhana ya ubaguzi wa kidini kuwa kigezo cha kuchaguliwa katika uongozi wa nchi, mwenzake Askofu Gwajima anatabiri kuwa mara tu baada ya kufanikiwa kushika hatamu za utawala, kitu cha kwanza kitakachotokea ni Misikiti kugeuka kuwa vituo vya kuwafundishia watoto imani ya Kikristo na Masheikh wote watapanga mistari kwenda kubatizwa kuwa Wakristo. Kwa maana nyingine Uislamu utafutika kabisa hapa nchini katika utawala wa Lowassa.

Ndugu wanahabari, Ushirikiano na ukaribu wa Lowassa na Askofu Gwajima si wa kuutazama kwa jicho moja tu. Tukumbuke kwamba ni Askofu Gwajima huyu huyu aliyekerwa kwa kuona Sehemu ya kuswalia Waislamu katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere wakati akieleza porojo zake za dhamira ya kujengwa Msikiti katika ofisi za Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG.

Ni Askofu Gwajima huyu huyu aliyekerwa na mchakato wa Mahakama ya Kadhi hadi akalazimika kutoa lugha zisizo na staha kwa watu wazima wakiwemo viongozi wakuu wa kidini hapa nchini.

kwa upande wake ndugu Lowassa huyu ndiye aliyefanikisha mkataba kati ya Serikali na Makanisa (MoU), mkataba ambao Waislamu tunaulalamikia mpaka leo hii.

Wanaposhirikiana wawili hawa pamoja na historia ya matukio yao hayo ya ‘KIBAGUZI’ kisha kila mmoja akatamka bayana maneno yanayotikisa misingi ya Utanzania na kuweka mbele ajenda zao za udini, si busara kuwanyamazia kwa maslahi ya Umoja wetu wa Kitaifa.

Haiwezi kuwa busara kwa Jamii ya Waislamu na watanzania wanaopenda amani, kukaa kimya wakati viongozi wa kisiasa na kidini kama walivyo Askofu Gwajima na Ndugu Lowassa wanatangaza hadharani nia yao ya kuivunja misingi ya utaifa na pia kukamia kuifuta dini yetu hapa nchini na kuwabatiza Masheikh nchi nzima, na kisha baada ya hapo kuigeuza Misikiti kuwa Sunday Schools za watoto wa kikristo. Hii ni dharau iliyochupa mpaka kwa dini tukufu ya Kiislamu na kwa waislamu wenyewe.

Ndugu Wanahabari, Taasisi yetu ya "Imam Bukhary Islamic Foundation" imekaa kimya kwa muda mrefu ikitafakari matukio hayo mawili ili kuona ni hatua gani stahiki zitachukuliwa kutokana na “cheche” hii ya moto wa hatari wa ubaguzi. Mwishowe tumeona tutahadharishe na kuwakumbusha Waislamu pamoja na Watanzania kwa ujumla yafuatayo:

(1) Kwa sauti ya juu Watanzania wote tumkemee na kumpinga Ndugu Edward Lowassa katika mpango wake wa kuona urais wa Tanzania unastahiki kwa zamu za Madhehebu ya dini, na tumwambie asiwagawe Watanzania kwa misingi ya kiimani

(2) Tuwakumbushe Ndugu Lowassa na Ndugu Gwajima kwamba Waislamu kamwe hawajasahau namna mchakato wa Mahakama ya Kadhi ulivyovurugwa kwa kuwatumia maswahiba wao, ambao leo hii wamejidhihirisha kuwa pamoja kwenye kambi zao za kampeni katika kuutafuta huo urais wa Tanzania, kwa dhana mbaya eti lau mchakato ule ungefanikiwa basi ungembeba mmoja kati ya wagombea wa urais.

(3) Tamko la Gwajima kuwa katika utawala ujao misikiti itageuzwa kuwa Sunday Schools za Watoto na Masheikh watakwenda kubatizwa na hivyo Uislamu kufutika hapa nchini, si tu kwamba ni maneno ya uchochezi, chuki na dharau kwa Waislamu, bali pia ni kipimo tosha kwa watanzania wote kutambua kuwa kundi hili halifai kiuongozi na ni wajibu wa kila mtanzania kumhadharisha mwenzake juu ya kumpigia kura Ndugu Lowassa na kundi lake.

(4) Kila Mtanzania anapaswa kufahamu kuwa, kumpigia kura Lowassa ni hatua moja katika kuvunja misingi ya amani na utangamano wa nchi yetu, kutokana na dhamira yake ya kuutazama uongozi wa nchi katika sura ya udini na umadhehebu. Lakini pia kila Mwislamu atambue kuwa kumpigia kura Lowassa itakuwa ni kuutimiliza utabiri wa Askofu

Gwajima wa kuwabatiza Masheikh wote Tanzania na kuigeuza Misikiti kuwa Sunday Schools kwa watoto wa kikristo.

Ni vizuri sisi Waislamu ambao ni waathirika wa mbinu chafu iliyotumika kuikwamisha Mahakama ya Kadhi, tumuulize Ndugu Lowassa: ameahidi kutatua kero kadhaa akiingia Ikulu, lakini kwanini hajapatapo kuitaja Mahakama ya Kadhi? Je, Lowassa hujui kuwa kutokuwepo kwa Mahakama ya Kadhi ni kero kwa Waislamu?

(5) Tuendelee kuhubiriana udugu wetu wa kitanzania na wale wote wenye nia mbaya tuwakemee na tuwazuwie kufikia kilele cha madaraka kitakachowawezesha kutimiza dhamira zao bila woga ili amani yetu idumu.

(6) Taasisi inajipanga kuandaa Semina maalum kwa Maimamu na baadhi ya Masheikh ili kujadili njia iliyo bora zaidi ya kujikinga na njama za wale wote ambao wanataka kulipasua Taifa letu kwa maslahi yao binafsi, wasifikie kwenye malengo yao hayo maovu.

Na tunawaomba Masheikh na Maimamu wa Misikiti yote Tanzania pamoja na Waislamu wote kushiriki kuwazindua Waumini kila pahala kote nchini kuwazindua Wananchi kwa ujumla juu ya hatari ya kuwaweka juu ya uongozi wa nchi yetu watu wenye dhamira ya kujenga dhambi ya ubaguzi wa kidini ambayo ni kansa itakayokula mwili wa Taifa na hatimaye kuliangamiza kabisa.

Ahsanteni kwa kunisikiliza.

Sheikh Khalifa Khamis
MWENYEKITI,
TAASISI YA KIISLAMU YA IMAM BUKHARY
(IMAM BUKHARY ISLAMIC FOUNDATION)
24/09/2015


CHANZO: JAMII FORUM

Wednesday, 15 July 2015

MATOKEO YA FORM SIX 2014/2015




MCHANGANUO  ULIOTUMIKA KATIKA MATOKEO HAYA

 1.    EXTINCTION  (DIV 1) =  FIRST CLASS  (UFAULU WA JUU)

2.     MERIT  (DIV 2)             =  UPPER SECOND CLASS (UFAULU MZURI)

3.    CREDIT  (DIV 3)            =   SECOND CLASS (UAULU WA WASTANI)

4.    PASS    (DIV 4)                =  LOWER SECOND (UFAULU WA KAWAIDA)

5. FAILURE   (ZERO 0 )       = AMEFELI 

Tuesday, 10 March 2015

MINISTRY OF EDUCATION AND VOCATIONAL TRAINING NEW ZEALAND COMMONWEALTH SCHOLARSHIPS

: 2015 AWARDS Applications are invited from qualified Tanzanians for Masters and Doctorate programmes for the 2015 New Zealand Commonwealth Scholarships under the Commonwealth Scholarship and Fellowship Plan (CSFP). QUALIFICATIONS Masters. Applicants for Masters’ degree must: • Have a Bachelor Degree with GPA of not less than 3.5 (this is not applicable for Health Sciences); • Be not than 35 years by February, 2016. Doctorate. • Have a Masters’ degree with GPA of not less than 4.0 or an average of “B” and above. • Be not more than 40 years by February, 2016. MODE OF APPLICATION  All applicants must fill in application forms which can be easily accessed from the following link: http://www.aid.govt.nz/funding-and-contracts/scholarships/eligible-countriesregions or you can goggle “application form New Zealand Commonwealth Scholarships 2015”  All applicants must seek and get admission from one of the Universities in New Zealand and they should attach a copy of admission notice with the filled application form.  All applicants must attach the Evidence from the Higher Education Students’ Loans Board to show that they have started repayment of the loans or completed paying the loans or they were not beneficiaries.  Applicants must ensure that they fulfill all requirements which are depicted on page 2 of the application form. All applications should be addressed to:- The Permanent Secretary, Ministry of Education and Vocational Training, P. O. Box 9121, DAR ES SALAAM and reach him not later than 15th June, 2015

Saturday, 21 February 2015

MATWEATHER AKUBALI KUZICHAPA NA PACQUIAO


Mwanamasumbwi raia wa Marekani Floyd Mayweather Junior ametangaza kuwa pigano lililosubiriwa kwa siku nyingi na mwanamasumbwi raia wa ufilipino Manny Pacquiao litafanyika mjini Las Vegas tarehe mbili mwezi Mei mwaka huu

Pambano hilo kati ya mabingwa hao wa unazi wa welterweight limekuwa likisubiriwa kwa miaka mitano.




Baada ya mazungmzo ya muda mrefu hatimaye kandarasi imetiwa sahihi.

Pigano hilo litakuwa la gharama kubwa zaidi ya historia ya dola milioni 250.

Wawili hao wanatajwa kuwa bora zaidi katika ndondi za uzani huo duniani.

habari kwa niaba ya BBC Swahili

HONGERA SIMBA WA AFRICA ROBERT MUGABE









Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ametimia miaka 91 leo.
Yeye sasa ni kiongozi mzee kabisa duniani, na amekuwa madarakani kwa miaka 35.
Sherehe ya siku yake ya kuzaliwa itafanywa juma lijalo.
Anatarajiwa kufanya sherehe kubwa katika uwanja wa golf huko Victoria Falls, inakisiwa sherehe yenyewe itagharimu dola milioni moja.

Maelfu ya watu watahudhuria karamu hiyo, ambapo kutachinjwa ndovu, nyati, paa na simba mmoja.
Shirika la habari la taifa linasema wananchi watalipia dhifa hiyo
Zimbabwe ni moja kati ya nchi maskini duniani.
HUYU NDIYE SHUJAA PEKEE WA AFRICA ALIYEBAKI BAADA YA MANDERA,NYERERE NA WENGINE WENGI WALITANGULIA KWA MOLA WAO.

habari kwa niaba ya BBC SWAHILI

Motisha kwa atakayefanikisha kukamatwa mtu anayejaribu kutorosha madini nje ya nchi


Wizara ya Nishati na Madini (WNM) inapenda kuutangazia umma kuwa kuanzia tarehe 15 Januari 2015, raia mwema yeyote atakayesaidia kukamatwa kwa mtu au kampuni yoyote inayojaribu kutorosha madini nje ya nchi kupitia mipaka yetu, bandari na viwanja vyote vya ndege nchini atazawadiwa.
Zawadi itakayotolewa ni fedha taslim ambazo ni sawa na asilimia 5 (5%) ya thamani ya madini yaliyokamatwa na kunadiwa. Thamani ya madini husika itapatikana kwa kutumia wataalamu wa madini walioidhinishwa <>

YAMOTO BAND INTERVIEW NA BBC DIRA YA DUNIA LONDON.

Yamotoni

Vijana wa Yamoto Band wakiwa na watangazaji Salim Kikeke na Charles Hillary
Tuliziona pichaz Yamoto Band pamoja na story za wao kwenda zao London, Uingereza kupiga show, siku ya leo FEB21 muda mfupi baadaye watakuwa na show, watu wetu hawa saa chache zilizopita walikuwa kwenye Interview na mtangazaji Charles Hillary kwenye BBC Dira ya Dunia.
Swali la kwanza kuulizwa ilikuwa wapi lilikozaliwa jina la Yamoto Band? ;”Ukiachana na vitu vya motomoto ambavyo tunavitoa ni jina ambalo lilibeba nyimbo yetu ya kwanza.. Yamoto Band ni zao la Mkubwa na Wanae, kituo ambacho kinalea watoto wenye vipaji..“– Aslay.
Kuhusu ishu ya mtu anayewaandikia nyimbo zao; “Mara nyingi sana tunaandika wenyewe lakini tunashare idea na bosi wetu Mkubwa Fella.. Tunakaa naye na tunashare idea“– Aslay.
Hapa wanaongelea utofauti wa Yamoto Band na band nyingine; “Vitu vingi vishafanyika, uongozi wetu unataka sisi tuwe wapya ndio maana bendi unaona iko tofauti kwanza tuna umri mdogo.. nyimbo zetu zina dakika tatu nne tofauti na bendi nyingine..“– Maromboso.
Band nyingi zinavunjika, unadhani hii itatokea kwa Yamoto?; “Sisi tumekaa ni zaidi ya miaka minne tuko pamoja kabla ya Yamoto Band kujulikana tunajua nini maisha halafu tumetoka katika maisha magumu.. Sio rahisi leo unishawishi kwa vitu vidogo milioni mbili milioni tatu wakati tunategemea mamilioni mengi baadaye“– Aslay.
Ni nini siri ya umoja wao?; “Tumekaa muda mrefu sana kwenye tundu moja kwa hiyo tumeshazoeana hata tabia zetu.. Tumeshakuwa kama ni ndugu sasa na sio marafiki tena“– Bella.
Hapa Charles aliomba kuambiwa maana ya ‘Kupwelepweta‘; “Kupwelepweta ni kitu ambacho hakikutoshi, kama mimi nivae koti lako lazima linipwelepete…“– Aslay.

NEW VIDEO: Madee (@Madeeseneda) ft. Chege (@ChegeChigunda) – VUVULA (Official Music Video)

http://djchokamusic.com/wp-content/uploads/2015/02/madee.jpg


NEW VIDEO: Chege (@ChegeChigunda) & Mh Temba Ft Dj Mapholisa – KAUNYAKA (Official Music Video)



NEW VIDEO: Jaguar (@RealJaguarKenya) – HUU MWAKA (Official Music Video)


NEW VIDEO: Jaguar (@RealJaguarKenya) – HUU MWAKA (Official Music Video)


NEW VIDEO: H.Mama ft AT – MKAZURURE (Official Music Video)


NEW VIDEO: BARNABA (@Barnabaclassic) & VANESSA MDEE (@VanessaMdee) – SIRI (Official Music Video)



#Siri tells the tale of a cunning young man who tries to convince a young bride to embark on a love affair with him, with promises of plenty material things. Despite her upbringing the story ends at a crossroads, leaving the listener wondering.
Artist: Barnaba Elias & Vanessa Mdee
Song Title: Siri
Composer: Barnaba Elias
Song Writer: Barnaba Elias & Vanessa Mdee
Publisher: Barnaba Elias & Vanessa Mdee
Producer: Mazuu
Video Director: Hanscana
For More: Barnaba
https://twitter.com/Barnabaclassic
https://www.facebook.com/VanessaMdee
http://instagram.com/barnabaclassic
www.barnababoy.com
Bookings:
Email: barnabaelias@gmail.com
Phone: +255682019955

For More: Vanessa Mdee
https://twitter.com/VanessaMdee
https://www.facebook.com/VanessaMdee
http://instagram.com/vanessamdee
www.vanessamdee.com

Email: vanessamdeemusic@gmail.com
Bookings:
Email: info@panamusiq.com
Phone: +255 784 172291







VIDEO: Show ya DIAMOND (@diamondplatnumz) kwenye Miaka 38 Ya Chama Cha Mapinduzi




Tuesday, 17 February 2015

FA Cup sixth-round draw: Manchester United to face Arsenal

 

League One’s Bradford City, who have knocked out Chelsea and Sunderland of the Premier League in the last two rounds of the FA Cup, have had their wish for a home tie in the sixth round granted with the visit of the Championship side Reading. The pairing ensures at least one Football League side will make it to the semi-finals.
Aston Villa take on West Bromwich Albion in a west Midlands Premier League derby while Liverpool’s hopes of reaching Wembley were boosted as they were drawn to face the Championship side Blackburn Rovers at Anfield.
Arsenal, the Cup holders, travel to Manchester United, who knocked out Preston in the fifth round on Monday.
All four games will be broadcast live by BBC or BT Sport. As lead broadcaster the BBC has first and third picks, with BT choosing second and fourth.

FA Cup sixth-round draw

Liverpool v Blackburn Rovers
Bradford City v Reading
Manchester United v Arsenal
Aston Villa v West Bromwich Albion

KOLO TOURE KUTUNDIKA DALUGA


Mlinzi wa timu ya Liverpool Kolo Toure ameuthibitishia ulimwengu kuwa anastaafu kusakata kabumbu la kimataifa akiwa na timu ya nyumbani Ivory Coast,wiki moja baada ya kuwasaidia Tembo hao kutwaa kombe la mataifa ya Afrika .
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka thelathini na tatu sasa, ameeleza wazi kuwa mchezo wake wa mwisho ni dhidi ya timu ya Equatorial Guinea hapo ndo mwisho wake kuonekana viwanjani.
Kolo anasema anaipenda nchi yake na hasa anachokipenda zaidi maishani mwake ni Kandanda,lakini akatanabaisha hufika wakati asitishe.
Kolo ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na chombo kimoja mjini Abidjan, Toure anasema najisikia vibaya sana kuwafahamisha kuwa niwakati wangu kuwaaga. Lengo0 langu lilikuwa kushinda katika michuano ya kombe la mataifa ya Africa, na nakubali ulikuwa ni uamuzi mgumu sana kuufanya.
Toure amekuwa kiungo muhimu sana katika kuutengeneza ushindi wa timu na taifa lake katika kipindi cha miaka ya 2006, 2010 and 2014 akiwa na kikosi cha timu yake ya taifa katika michuano ya kombe la dunia..
Ametua katika michuano ya kombe la mataifa ya Afrika mara saba ,akiwa amekosa penati mbili katika mechi mbili za fainali dhidi ya Egypt mwaka 2006 na ingine ni ile ya Zambia mwaka 2012 kama unakumbuka vyema.
Koro kazini enzi hizo.
Mchezaji huyo nguli ambaye amesukuma gozi kwa miaka kumi na mitano uwanjani akiwa mchezaji wa kimataifa na anamuacha meneja wa timu yake ya Ivory Coast Herve Renard akiwa na tabasamu tele katika kumtafuta mrithi wa Kolo
Na kolo amemtaja mrithi wake kuwa ni Ousmane Viera Diarrassouba, ambaye atakaba nafasi ya ulinzi baada yake.
Nadai huwa hafanyi makosa pindi afanyapo uchaguzi wa nani akae wapi, naamini mrithi wangu atawapika vyema vijana wawili Eric Bailly na Wilfried Kanon.na hivyo anaamini Viera atamuwakilisha vyema.
Kolo alianza kuonesha cheche zake katika timu ya ASEC Mimosas ya Abidjan, Toure kisha akaelekeza daluga zake kwenye timu ya Arsenal mnamo mwaka 2002 na alikuwa chachu ya kutofungwa kwa msimu wa miaka miwili mfululizo nazungumzia miaka ya 2003/4.
Lakini baadaye alimwaga wino katika kilabu cha Manchester City mnamo mwaka 2009 kabla hajaelekea katika timu ya Liverpool kwa uhamisho wa bure msimu uliopita.

Habari kwa hisani ya BBC Swahili.

Sunday, 15 February 2015

Diamond Ft P - Square - Nakupenda [Audio]




Tanzania has embarked on the implementationTANZANIA HAS EMBARKED ON THE IMPLEMENTATION FOR THE SIX FLYOVERS IN DAR ES SALAAM AIMING TO DECONGEST THE CITY


Tanzania has embarked on the implementation for the construction of six flyovers in Dar es Salaam, aiming to decongest the city.
“The country is currently undergoing the challenges of congestions and in order to address that we are planning to build at least six flyovers and overheads roads,” the Tanzania National Roads Agency (TANROADS) chief executive officer, Mr. Patrick Mfugale said, adding that six areas have been identified where there are road junctions.
He said the flyovers will be built at Tazara, Ubungo, Magomeni, Fire, Kamata and Chang’ombe road junctions.
According to Mr. Mfugale, the construction of the first flyover at Tazara Intersection where Nyerere Road crosses Nelson Mandela Road is expected to commence in September this year following a grant of Tsh 52.2 billion ($ 32.6 million) that was issued by Japan.
Tanzania and Japan have already signed a grant of Tsh 1.1 billion ($ 688,261), for the detailed design of the flyover project which is expected to be complete at the end of July this year.
Mr. Mfugale explained that once the design is complete, Japan will announce tender for a contractor in their country an exercise that is expected to be completed within three months.
“Once the tender process of finding a contractor from Japan is completed we expect to take off construction in September,” he said.
However he declined to mention the time frame of the construction because it will be determined by the design which is yet to be completed.
“This fly over will contribute to alleviating the existing traffic jams in Dar es Salaam, as well as to strengthening the role of the Tanzanian road network as an international corridor connecting Dar es Salaam Port and the nearby land-locked countries,” he said.
Mr. Mfugale explained that the next construction is the Magomeni junction flyover that is expected to take off as soon as funds are allocated.
According to him, fund is the barrier and they were currently initiating for the implementation of detail designs to determine the cost of the flyovers.
The government of Tanzania has allocated Tshs 28.6 million ($ 17 million) in this year’s fiscal budget to address the problems of congestion in Dar es Salaam city.
The funds will be used for upgrading the city roads while Tshs 1,000 million ($ 625,692) will be injected in the construction of the Tazara flyover.
The Tazara flyover at the junction of Nyerere Road and Mandela Expressway would have a big impact on the socio-economy because it was aimed at reducing congestion in Dar es Salaam.
Alleviating traffic congestion has huge potential to contribute the national economic growth. Dar es Salaam  city that continues to grow and become increasingly commercial destinations and activities, so is the starting point for all transport systems, including road, rail, air and maritime transport systems.
Since  Dar  es  Salaam  is  the metropolis  of  Tanzania  accounting  for  more than 60% of national tax revenue of the country as  a  whole,  congestion  has  a  huge  impact  on the economy.
According to TWAWEZA (2010) report, reveal Nine Solutions to Ease Congestion in Dar es Salaam including Different Vacation Periods that it could be decided that school vacations do not all take place at once.
“They could be split into periods of a few weeks, with every zone starting their vacation on different dates,” the report reads.
Another solution is Restrict Cargo Traffic mean that  restrict  the  movement  of  large  (exceeding  10 tons)  trucks  on  busy  route,  with  high  traffic, such  as  Bagamoyo,  Morogoro,  Nyerere  and Mandela  roads.
TWAWEZA says Restrict Traffic Entry points is another solution whereby cars  should  be  allowed  to  enter  main  stream traffic  only  via  select  roads/streets,  with  no exiting  or  entering  traffic  less  than  100m  from any  major  traffic  junction.
It says Redirected traffic, double lanes is also a solution which by use uncongested inner-most lane to ease a congested side. This  can  be  used  everywhere when  double  lanes  are  available  and  only  one side  is  congested,  with  one  traffic  policeman after each 200m between junctions. 
Others are Passenger-friendly Bus Transport and Priority traffic for buses.
“Other  traffic  should  be  allowed only  when  moving  at  speeds  greater  than  70 kilometer per hour” it shows.

BY.Corporate-digest

UTARATIBU WA KUTUNUKU MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE NA CHA SITA KWA KUTUMIA MFUMO WA GPA

1. Mfumo wa Wastani wa Pointi (Grade Point Average - GPA)

Huonesha wastani wa pointi alizopata mtahiniwa katika masomo aliyofaulu katika mtihani wake.
GPA hutokana na masomo saba (07) aliyofaulu vizuri zaidi mtahiniwa katika Mtihani wa Kidato cha Nne na masomo matatu (3) ya tahasusi katika Mtihani wa Kidato cha Sita. Mtahiniwa aliyefanya masomo pungufu ya 07 kwa CSEE au pungufu ya 03 kwa ACSEE, atafaulu katika kiwango cha “Pass” endapo atapata angalau Gredi D katika masomo mawili au gredi C, B, B+ au A katika somo moja.

Uzito wa Gredi A= 5, B+ = 4, B = 3, C = 2, D = 1, E = 0.5 na F = 0.

Utaanza kutumika kupanga madaraja ya ufaulu katika Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) 2014 na Kidato cha Sita (ACSEE) 2015.

2. Ukokotoaji wa GPA ya Mtahiniwa
Hufanyika kwa kuchukua jumla ya uzito wa gredi katika masomo saba (07) aliofanya vizuri kwa Mtihani wa Kidato cha Nne na matatu (3) ya tahasusi kwa Mtihani wa Kidato cha Sita na kugawanya kwa idadi ya masomo. Ukokotoaji huo huzingatia kanuni ifuatayo:

GPA =
Jumla ya Uzito wa gredi za masomo
------------------------------------------------
Idadi ya Masomo

Masomo yatakayotumika katika ukokotoaji wa GPA ya mtahiniwa ni yale ambayo amefaulu; yaani amepata Gredi A, B+, B, C au D.

3. Muundo wa Madaraja Kwa Kutumia Mfumo wa GPA
Katika mfumo wa Wastani wa Pointi (GPA) kutakuwa na madaraja manne ambayo ni Distinction, Merit, Credit na Pass.

 ........................................................................................................................................

Daraja la juu la ufaulu ni Distinction na la chini ni Pass kama ilivyoainishwa katika Jedwali lifuatalo:
 

Mfano; Mtihani wa Kidato cha Nne, mtahiniwa aliyepata ufaulu wa Civics (A), History (B+), Geography (B+), Kiswahili (B), English (C), Physics (C), Chemistry (C), Biology (C) na Mathematics (E) atakuwa na jumla ya pointi 22 kwenye masomo saba aliyofanya vizuri.

Idadi hiyo ya pointi ikigawanywa kwa idadi ya masomo saba (07), Mtahiniwa huyu atakuwa na Wastani wa Pointi (GPA) 3.1 na atatunukiwa daraja la Merit. Katika Mtihani wa Kidato cha Sita mtahiniwa aliyepata ufaulu wa Physics (A), Chemistry (B+), Biology (A), Basic Applied Mathematics (D) na General Study (A) atakuwa na jumla ya pointi 14 kwenye masomo ya tahasusi (PCB). Idadi hiyo ya pointi ikigawanywa kwa idadi ya masomo matatu (03), mtahiniwa atakuwa na Wastani wa Pointi (GPA) 4.7 na atatunukiwa daraja la Distinction.

4. Manufaa ya kutumia Mfumo wa Wastani wa Pointi (GPA);
Kuwa na mfumo wa kutunuku matokeo wa aina moja katika ngazi zote za mafunzo kuanzia Elimu ya Msingi hadi Elimu ya Juu;

Matokeo yaliyo katika mfumo wa wastani wa pointi kwenye cheti yatarahisisha kazi ya udahili wa watahiniwa unaofanywa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) katika ngazi za juu za mafunzo na Mfumo wa wastani wa pointi (GPA) ni rahisi kueleweka kwa wadau wa kada mbalimbali kwa sababu hutoa tafsiri yenye kuonesha mtahiniwa aliye na GPA kubwa ndiye aliye na matokeo mazuri kuliko aliye na GPA ndogo.

Maelezo zaidi kuhusu GPA yanapatikana katika tovuti ya Baraza la Mitihani (www.necta.go.tz).
 


Ufaulu Kidato cha Nne 2014 wapanda kwa asilimia 10

Jumla ya Watahiniwa 196,805 sawa na 68.33% ya watahiniwa wote waliofanya mtihani kidato cha IV mwaka 2014 wamefaulu ikiwa ni ongezeko la 10.08% kulinganisha na mwaka 2013 ambapo wanafunzi 235,227 sawa na 58.25 walifualu.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa Dkt Charles Msonde
Jumla ya Watahiniwa 196,805 sawa na 68.33% ya watahiniwa wote waliofanya mtihani kidato cha IV mwaka 2014 wamefaulu ikiwa ni ongezeko la 10.08% kulinganisha na mwaka 2013 ambapo wanafunzi 235227 sawa na 58.25 walifualu.

Akitangaza matokeo ya Kidato cha Nne ya mwaka 2014 leo jijini Dar es salaam, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa Dkt Charles Msonde amesema kati ya waliofaulu, wasichana ni 89,845 sawa na asilimia 66.61 wakati wavulana ni 106,960.

Amesema watahiniwa wa shule waliofaulu ni 167,643 sawa na asilimia 69.76 ya waliofanya mtihani, wasichana wakiwa 75,950 sawa na asilimia 68.70 na wavulana 91,693 sawa na asilimia 70.67.

Amesema mwaka 2013 watahiniwa 201,152 sawa na asilimia 57.09 ya watahiniwa wa shule walifaulu mtihani huo hivyo ufaulu kwa wanafunzi wa shule umepanda kwa asilimia 12.67 mwaka 2014 ikilinganishwa na mwaka 2013.

Akizungumzia ubora wa ufaulu, Dkt Msonde amesema kuwa jumla ya watahiniwa waliopata ufaulu mzuri wa madaraja ya Distinction, Merit na Credit ni 73,832 sawa na asilimia 30.72 wakiwemo wasichana 27,991 sawa na asilimia 25.32 na wavulana ni 45,841 sawa na asilimia 35.33.

Watahiniwa waliopata daraja la PASS 93,811 sawa na asilimia 39.04 na waliofeli kwa kupata daraja la FAIL 72,667 sawa na asilimia 30.24.
Kuhusu ufaulu wa masomo, Dkt Msonde amesema kuwa ufaulu katika masomo ya msingi umepanda kwa kati ya asilimia 1.28 na 11.22 ikilinganishwa na mwaka 2013.

Ufaulu wa juu kabisa umekuwa katika somo la Kiswahili ambapo asilimia 69.66 ya watahiniwa wote wamefaulu na ufaulu chini kabisa ni wa somo la Basic Mathematics ambapo asilimia 19.58.

Amesema Baraza limefuta matokeo ya watahiniwa 184 baada ya kubainika kufanya udanganyifu, kati yao 128 ni watahiniwa wa kujitegemea na 56 ni watahiniwa wa shule.

Akizitaja shule kumi bora kwa ufaulu


Dkt Msonde amesema shule hizo ni;
Kaizirege mkoa wa Kagera
Mwanza Alliance mkoa wa Mwanza
Marian Boys mkoa wa Pwani
St. Francis Girls mkoa wa Mbeya
Abbey mkoa wa Mtwara
Feza Girls mkoa wa Dar es salaam
Bethel sabs Girls mkoa wa Iringa
Marian Girls mkoa wa Pwani
Feza Boys mkoa wa Dar es laam.

Shule 10 za mwisho ni;
Manolo mkoa wa Tanga
Chokocho mkoa wa Pemba
Kwalugulu mkoa wa Tanga
Relini mkoa wa Dar es salaam
Mashindei mkoa wa Tanga
Njelekela Islamic Seminary mkoa wa Kigoma
Vudee mkoa wa Kilimanjaro
Mnazi mkoa wa Tanga
Ruhembe mkoa wa Morogoro
Magoma mkoa wa Tanga.

Dkt Msonde pia ametaja watahiniwa 10 waliofanya vizuri kuwa ni;
Nyakaho Marungu kutoka Baobab Pwani
Elton Sadock Jacob kutoka Feza Boys Dar es salaam
Samwel M Adam kutoka Marian Boys Pwani
Fainess John Mwakisimba kutoka kutoka St Francis Girls Mbeya
Mugisha Reynold Lukambuzi kutoka Bendel Memorial Kilimanjaro
Paul W Jijimya kutoka Marian Boys Pwani
Angel Lundgreen Mcharo kutoka St Francis Girls Mbeya
Atuganile Cairo Jimmy kutoka Canossa
Jenifa Lundgreen Mcharo kutoka St Francis Girls Mbeya
Mahmoud Dadi Bakili kutoka Feza Boys.
 
Habari kwa hisani ya Jamii forum.com 

Saturday, 14 February 2015

BREAKING NEWS MATOKEO KIDATO CHA NNE HAYA HAPA


BOFYA HAPA KUPATA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2014 KWA SHULE ZOTE

 

 

 

MCHANGANUO  ULIOTUMIKA KATIKA MATOKEO HAYA

 1.    EXTINCTION  (DIV 1) =  FIRST CLASS  (UFAULU WA JUU)

2.     MERIT  (DIV 2)             =  UPPER SECOND CLASS (UFAULU MZURI)

3.    CREDIT  (DIV 3)            =   SECOND CLASS (UAULU WA WASTANI)

4.    PASS    (DIV 4)                =  LOWER SECOND (UFAULU WA KAWAIDA)

5. FAILURE   (ZERO 0 )       = AMEFELI 


SHULE 10 BORA 2014
1.Kaizirege-Kagera
2.Mwanza Alliance-Mwanza
3.Marian boys-Pwani
4. St. Francis-Mbeya
5.Abbel-Mtwara
6.Feza Girls
7.Canossa-Dar
8.Bethel Sabs Girls-Iringa
9. Marian Girls-Pwani
10.Fedha Boys


SHULE 10 ZILIZO HARIBU 2014

1.Manolo-Tanga
2.Chokocho-Pemba
3.Kwaluguru-Tanga
4.Relini-Tanga
5.Mashindei-Dar es Salaam
6.Njelekela Islamic Seminary-Kigoma
7.Vudee-Kilimanjaro
8.Mnazi-Tanga
9.Ruhembe-Morogoro
10. MAGOMA-Tanga


Wednesday, 11 February 2015

KIBA NA CRISS BROWN NDANI YA NGOMA MOJA SOON

 http://www.aitonline.tv/pix/NewsImages/4108.jpg
Uongozi wa muziki nchini marekani unao muongoza msanii wa R&B Chris Brown umetoa taarifa kwa uongozi wa muziki Tanzania unao muongoza msanii kutoka Tanzania ALI KIBA msanii ambae yupo chini ya uongozi wa Kampuni za SAMSUNG....


Kwa taarifa zilizopo katika mtandao wa VIP Beats nchini marekani zinaeleza kua tarehe 24 mwezi wa 11 mwaka 2014 uongozi wa msanii Chris Brown ulipokea maombi ya muungano wa wasanii wawili kufanya wimbo wa pamoja kati ya msanii Ali kiba na Chris Brown maombi hayo yaliambatanishwa na Softcopy zilizobeba nyimbo tatu za msanii Ali kiba ikiwemo SINGLE BOY,

MWANA pamoja na wimbo aliofanya katika project ya ONE 8. Uongozi wa Chris Brown umethibitisha kupokea taarifa za maombi hayo na umeonesha kupenda sauti ya msanii Ali kiba na kutoa tamko kua wapo tayari kusimamia kazi ya pamoja itakayofanywa na wasanii hawa.

Upande wa msanii Chris Brown amesema hana tatizo yupo tayari kushirikiana na msanii Ali kiba kwani alipata nafasi ya kutazama project ya One 8 na ameona kiwango cha msanii Ali kiba kinaridhisha

Japokua anahitaji marekebisho madogo sana. BBC SWAHILI Tunampongeza msanii Ali kiba kwa juhudi zake tunamtakia kila lakheri katika kazi hii, kuipata habari hii kamili tembelea mtandao wa VIP Beats, Channel 0 au unaweza kuipata katika American Spring news.
Breaking News
Loading...

Search This Blog

LIKE PAGE ZETU ZA FACE BOOK

ZINGINE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...