MICHONGO KAMILI

Monday, 30 December 2013

NEY WA MITEGO NI FREEMASSON?

 FREEMASSON NA NEY WA MITEGO !!!!!!!
Blog hii kwa mara ya kwanza imeamua kukuletea jambo ambalo limekuwa gumzo sana midomoni mwa watu.......ni kuhusu uwepo wa dini ya kishetani iitwayo freemasson,inasemekana kuwa  uwepo wa dini hii ume kuwa ni wa kificho sana ....lakini kwa ushahidi mbakli mbali inaonyesha kuwa dini hiyo ipo na ina endesha shughuri zake ulimwengu mzima... ushahidi mmoja wapo ni uwepo wa freemasson hall mjini dar es salaam maeneo ya posta ambalo ni hili hapa chini kama lionekanavyo kwenye picha..
inasemekana dini hiyo imekuwa ikiwashawishi wasanii wakubwa ambao ni kioo cha jamii ili kujiunga na dini hiyo ili kuwa poteza mashabiki wa msanii hao, baadhi ya wasanii wamewa wakitajwa kujihusisha na dini hiyo majina kama DIAMOND PLATNUMZ  na  NEY WA MITEGO yamekuwa yakitamkwa sana mitaani huku yakihusishwa sana na dini hiyo huku sababu kubwa ikiwa ni matendo yao,maneno,skendo,na alama tofauti tofauti ambazo wamekuwa wakizionyesha kwenye mausha yao ya muziki,,,,,,,je   kuna  ukweli  wowote? kwa leo  tutaanza  na ushahidi kadhaa uliokusanywa na blog hii kuhusu msanii ney wa mitego....
Ney wa mitego ametokea kuwa nsanii aliye teka sana soko la muziki wa hip hop hivi karibuni lakini amekuwa akipunguza mashabiki kutokana na skendo mbalimbali kama hii inayo onekana hapa chini.

Tukiachana na skendo hizo bado kume kuwa na alama mbali mbali ambazo msdanii huyo amekuw akizionyesha kwenye video zake huku aki tamka maneno ambayo yana mtambulisha yeye kama rafiki wa dini hiyo kwa mfano kwenye nyimbo yake maaru iitwayo "NASEMA NAO" alimetoa sentensi kadhaa ambazo zina dhihirisha uhusika wake katika dini hi yo kwa mfano aliposema "unataka kwenda mbinguni huwezi fika bila mii" swali ni kwamba  yeye ni nani???? pia  mstari mwingine ni ule usemao "mimi ndo rafiki wa lucifer !! utanieleza nini " yeye ni rafiki wa LUCIFER  na lucifer ni mungu wa dini hiyo kama anavyo onekana hapa chini
pia amekuwa akionyesha alama mbali mbali ambazo ni alam,a za dini hiyo kama inavyoonekana hapa chini
hakuishia hapo pia katika video yake iitwayo "NASEMA NAO" ameonyesha alama hizo mara nyingi zaidi na kwakukusudia kabisa kwa mfano katika picha zifuatazo

je hii ni bahati mbaya? au ni swaga kama wasemavyo vijana wa mjini ambao wamekumbwa na mkumbo huo wa kuiga matendo ya wasanii wakubwa huku wakiita swaga!!!!!!! tuendelee!!

je na hii ni bahati mbaya? au bado ni swaga? sijui!!

  hatuhitaji kutumia miwani kuona alama hizi !!
huu ni ushahidi tu uliokusanywa na blog hii na halazimishwi mtu kukubaliana na ushahidi huu....
mhhhhhhhhhhhhhhhhh!!!!!!!
mwishoni mwa nyimbo hiyo anasema hivi  "I represent my hood" lakini badala ya kuonyeshwa manzese anaonyeshwa akiwa na watu kadhaa ambao wamevaa mavazi ya kufunika ambayo inaaminika kuwa hutumika katika ibada za freemasson je? ana represent manzese au makundi ya watu hao? kilichoonyeshwa ni hiki!!!

haya ni mambo kadhaa tu anayo yafanya msanii huyun  nakufanya wengi waamini juu ya uhusika wake kwa dini hiyo ya FREEMASSON   Lakini vipi kuhusu DIAMOND?
Acha blog hii ikusanywe kwanza kisha itarudi jamvini kuwapasha yaliyomo!!!   ALLEVIDEH!

Tuesday, 3 December 2013

Viongozi wa jumuiya ya afrika mashariki waliokutana mjini Kampla Uganda wametia saini sheria ya makubaliano ya kuwa na sarafu ya pamoja.



Kutiwa saini kwa makubaliano hayo ni hatua muhimu ya kukuza mshikamano wa jumuiya hiyo yenye nchi tano.
Makubaliano hayo ya kisheria yalitiwa saini na viongozi wote watano wa jumuiya ya afrika mashariki kwenye kongamano la 15 lenye maudhui ya kuwa na sarafu moja.
Akizungumza kwenye kongamano hilo katibu mkuu wa jumuiya ya Afrika mashariki bwana Richard Sezibera anasema kubuniwa kwa mkataba wa kuwa na sarafu moja ni hatua muhimu ya mshikamano haswa baada ya kuwa na soko la pamoja na umoja wa forodhani ambazo zinasaidia usafirishaji wa bidhaa na mitaji.
"Eneo letu linapiga hatua kubwa ya mshikamano haswa baada ya kutiwa saini kwa makubaliano ya kuwa na sarafu moja. Umoja huu wa sarafu unaiweka jumuiya yetu kwenye awamu nyingine na ni hatua muhimu. Kutiwa saini kwa makubaliano Haya pia ni mwamko mpya wa mshikamanno wa kifedha."
Kutiwa saini kwa sheria hii ya sarafu moja kunatoa nafasi kwa nchi wanachama kuanza kuondoa sarafu zao za ndani ya nchi ili baadaye kuanza kutumia sarafu ya pamoja kote kwenye jumuiya ya afrika mashariki.
Mwenyekiti mpya wa jumuiya hiyo ambaye ni Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta anaiona hii kama hatua muhimu ambayo itavutia zaidi wawekezaji kwenye eneo la afrika mashariki.
"Wafanyi biashara watapata Uhuru zaidi wakufanya shughuli zao huku nao wawekeaji wakiongezeka wakipata fursa bora ya kuja kwenye kanda hii. Tukiwa na manufaa kama hayo bila shaka uwekezaji utaongezeka na kuboresha uchumi wetu"
Chini yasheria hii nchi wanachama wa EAC wanatakiwa kuwasilisha sera zao za kubadilisha fedha kwenye benki kuu ya afrika mashariki itakayobuniwa, hii ikiwa ni hatua za kuelekea kuwa na sarafu ya pamoja.
Wajibu wa benki hiyo kuu ya afrika mashariki itakuwa ni kuthibiti dhamani ya sarafu moja na pia kusimamia maswala yote ya kifedha kwenye kanda.
Lakini ingawa viongozi wa afrika mashariki wanaisifu hatua hii ya sarafu moja na kuitaja kuwa yenye manufaa kwa mshikamano, wataalam wanahoji kwamba bado kuna maswala muhimu kuliko kuwa na umoja wa sarafu kama vile biashara baina ya nchi wanachama.
Bwana Louis Kasekende ni naibu gavana wa benki kuu ya Uganda.
"Sitaki tuzingatie kupita kiasi kuwa na sarafu ya pamoja. Lazima pia tuzingatie mambo ambayo tungependa kufanikishsa Kama vile maswala ya maendeleo ya kiuchumi. Tunahitaji kufanya biashara zaidi kwa kuuza bidhaa na huduma miongoni mwetu."
Lakini Gavana wa benki kuu ya Tanzania Profesa Benno Ndulu ana maoni tofauti.
"Tutakuwa tu na sarafi moja kwa hiyo inarahisisha sana biashara na inarahisisha pia kuwa na soko moja kubwa"
Tayari jumuiya ya afrika mashriki imefanikiwa kubuni soko la pamoja na umoja wa forodha hali ambayo imeimarisha biashara kufuatia kuondolewa kwa vikwazo vya barabarani na pia mipakani.
Nchi zote tano zina zaidi ya watu million 135 na kwa pamoja zina pato la jumla la dola bilioni 85.

Mkataba huu wa sarafu moja uliotiwa saini leo utatekelezwa ndani ya miaka kumi na hapo ndipo jumuiya ya afrika mashariki itaanza kutumia pesa moja tu.

NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI KUTUMIA SARAFU MOJA BAADA YA MIAKA 10

NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI KUTUMIA SARAFU MOJA BAADA YA MIAKA 10
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6HV-LW830SD6AESsqbWZBWw3W6BPQpPw-32PrjPAUbyNf6DPK3oK_hoIVvFmMoGAGC3AqmK07AtmWT84jKi2UXJmwef71-5rLiV0j3gd5UlyvA4j3vFbMigUV6J971bQagFN5sc_yWg9y/s640/MONETA.jpg
Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) anayeshughulikia Miundombinu,Dk Enos Bukuku akizungumza na waandishi wa habari jijini Kampala leo juu ya hatua zilizofikiwa katika kuweka saini Itifaki ya Sarafu Moja jumamosi wiki kwenye Uwanja wa Kololo nchini Uganda,kushoto ni Mkufunzi na Mwandishi Mkongwe,Jenerali Ulimwengu.

Na Mwandishi Wetu,Kampala

Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jumamosi wiki wameweka saini Itifaki ya Sarafi Moja ikayowezesha matumizi ya Sarafu moja katika nchi hizo.

Matumizi ya Sarafu moja yatachukua muda kutekelezwa  ili kutoa nafasi ya utekelezaji wa michakato mbalimbali ya kuoainisha sera na sheria ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa taasisi kadhaa kabla ya kuanza kutumika Sarafu hiyo inaweza  kuchukua miaka 10.

Akizungumza na waandishi wa habari leo ,Naibu Katibu Mkuu wa EAC anayehusika na Miundombinu,Dk Enos Bukuku amesema utaratibu huo utazifanya nchi wanachama kukubaliana katika mambo ya sera za fedha za Jumuiya hiyo na kuwa na Benki Kuu ya EAC.

Amesema wataalamu katika Sekretariat ya Jumuiya hiyo wamekua wakienda kujifunza mfumo wa utendaji kazi wa Sarafu moja kwenye nchi za Umoja wa Ulaya(EU). 

Saturday, 23 November 2013

GAZETI LA AMANI NI NOMA KWAKUCHIMBA 
Diamond kwa sasa ndiye mwanamuziki aliye matawi ya juu zaidi kuliko yeyote kwenye Bongo Fleva, akisumbua vibaya na kibao chake cha Number One wakati Penny akiingiza mkwanja kupitia utangazaji katika kituo cha Runinga ya Dar es Salaam ‘DTV’.
ISHU YABUMBURUKA!
Sosi wa karibu, ndani ya familia ya Diamond alinyetisha kwamba, Diamond na Penny ni ndugu wa damu lakini jambo hilo limefahamika hivi karibuni na hivyo wanahaha namna ya kuzima aibu hiyo.
Kwa sharti la kutochorwa jina gazetini, sosi huyo alisema: “Ndugu kwenye familia wanagongana. Wanajaribu kufichaficha hili jambo, lakini inashindikana. Unajua kinacholeta shida zaidi ni kwamba Diamond na Penny watakavyokuwa baada ya uamuzi kupitishwa.”
Alisema, pamoja na ukweli huo kugundulika bila shaka kuwa ni ndugu, bado kuna ugumu wa wapenzi hao waliozama kwenye dimbwi la mahaba kisha kuvunja amri ya sita, kuachana na kubaki wakiheshimiana kama kaka na dada.
“Tatizo ni je, Diamond atakubali kumchukulia Penny kama ndugu yake? Kama atakubali na Penny naye atakuwa tayari? Wote kwa pamoja wanaonekana kama wanapingana na jambo hilo,” alisema.
UNDUGU WENYEWE UKOJE?
Akieleza aina ya unasaba wa Diamond na Penny, sosi wetu huyo alisema, bibi mzaa mama wa Diamond na bibi mzaa mama wa Penny, wamezaliwa na mama mmoja.
Hapa anafafanua: “Kwa sababu hiyo sasa, unaweza kuona kuwa, wale ni sawa tu na mtu na kaka yake. Tena wako ndani ya ukoo kabisa, sema hao mabibi, kila mmoja alikuwa na baba yake, walichangia mama tu.
“Familia imejiridhisha kabisa, halafu isitoshe imeonekana kuwa, undugu wa kuchangia mama ndiyo wa uhakika zaidi kuliko wa baba ambao mtu anaweza kubambikwa hata mtoto asiye wake. Kifupi Penny na Diamond ni ndugu. Sema ndiyo hivyo historia za wazazi wao zinashangaza mpaka basi.”
Kwa mujibu wa sosi wetu, majina ya bibi hao wanaounganisha undugu ni Khadija Said Abas (bibi yake Penny) na Tatu Omar (bibi yake Diamond), wote kwa sasa wametangulia mbele ya haki.
“Kinachoshangaza sasa, mama Diamond amefurahi sana na amezidisha mapenzi yake kwa Penny, ndiyo maana hataki kusikia mwanaye anakuwa na mwanamke mwingine zaidi ya Penny.
“Mwenyewe anasema, kwanza undugu siyo wa karibu sana hivyo haina madhara lakini pia anajua Diamond atampenda, kumheshimu na hatamnyanyasa kwa sababu ni sehemu ya damu ya familia yao,” sosi aliendelea kutiririka.
HAPA AMANI, KULE DIAMOND
Amani lilifanya juhudi za kumsaka Diamond katika simu zake zote za mkononi bila mafanikio, likahamia kwenye mitandao ya kijamii, likamnasa ambapo awali mahojiano yalikuwa na kigugumizi lakini baadaye mambo yalikuwa hivi;
AMANI: Mzee vipi, mbona hupatikani kwenye simu zako zote? Kuna jambo nataka kukuuliza bwana mkubwa.
DIAMOND: Niko Nigeria. Vipi, kuna nini tena?
AMANI: Kuna stori fulani... eti ni kweli bibi yake Penny mzaa mama na bibi yako wewe ni ndugu wa damu kwa maana wamezaliwa na mama mmoja?
DIAMOND: Yeah but wamechangia mama, kila mmoja na baba yake.
AMANI: Kwa hiyo Penny ni dada yako kiasili si ndiyo?
DIAMOND: Yap!
AMANI: Duh! Majanga... kwa hiyo unatembea na dada yako wa damu?
DIAMOND: Nilikuwa najua basi kaka?!
AMANI: Kwa hiyo sasa baada ya kugundua hivyo, unaachana naye au?
DIAMOND: Kama nilivyokuambia, niko Nigeria... halafu niko gym sasa hivi, nitakutafuta nikitoka.
AMANI: Sawa, naomba ujibu hili swali la mwisho. Tumesikia kuwa, mama yako anampenda sana Penny, ni kwa sababu amegundua kuwa una undugu naye?
DIAMOND: Ha! Ha! Ha! Nikitoka gym nitakupigia simu tuzungumze vizuri.
Diamond hakufanya hivyo. Hata alivyotafutwa baadaye kwenye mtandao huo, pia hakuonekana kuwa hewani.
PENNY MIKONONI MWA AMANI
Penny alipopatikana juzi Jumanne, kwa njia ya simu alielezwa ilivyo ambapo alisema: “Ni kweli Diamond ni ndugu yangu wa damu. Tumegundua tukiwa tayari tumeshakuwa wapenzi.
“Hakuna jinsi tena, sanasana naona kama mapenzi yetu ndiyo yamezidi kuimarika. Nampenda sana Diamond wangu na sababu hiyo haitoshi kututenganisha maana kama ni makosa tayari yameshatokea.”
MAMA DIAMOND
Kwa upande wake mama Diamond, baada ya kusimuliwa kila kilichofika mezani mwa Amani na kutakiwa kueleza msimamo wake alijibu kwa kifupi: “Ndiyo ni kweli unayosema, lakini kwa sasa nipo huku Kariakoo (Dar), sipo kwenye nafasi nzuri ya kuzungumza. Njoo nyumbani jioni, tuzungumze vizuri.”
Diamond na Penny wamekuwa kwenye penzi lenye kasheshe nyingi kufuatia mwanamuziki huyo kuhusishwa na wanawake wengine akiwemo aliyekuwa mpenzi wake wa zamani, Wema Isaac Sepetu.


MAJANGA REMIX YA DOGO SKIDE

Sunday, 20 October 2013

WATANI WA JADIIII! NA HAYA NDIO YALIYO TOKEA

DAKIKA 14:SIMBA 0 - YANGA 1 MFUNGAJI   MRISHO NGASA

DAKIKA YA 20 :SIMBA 0 - YANGA 1

DAKIKA YA 35 :SIMBA 0 - YANGA 2 MFUNGAJI HAMISI KIIZA

DAKIKA YA 47 SIMBA 0 - YANGA 3  MFUNGAJI HAMISI KIIZA

HALF TIME  SIMBA 0 - YANGA 3
DAKIKA YA 53 SIMBA 1 - YANGA 3 MFUNGAJI BETRAM MWOMBEKIBETRAM

DAKIKA YA 57 SIMBA 2 - YANGA 3 MFUNGAJI JOSEPH OWINO

SIMBAAAA!!!!DAKIKA YA 83 SIMBA 3 - YANGA 3 MFUNGAJI  GIRBERT KAZE
SASA KWANINI MASHABIKI WA YANGA WASISHIKE KICHWA
KWA KUPOKONYWA  TONGE MDOMONI

NA HII NI NGOMA YA MWANADADA RECHO AMBAYO IMETOKA SAMBAMBA NA NGO YA MWADADA LINAH

HII NDIO NGOMA MPYA YA MWANA DADA LINAH! INAYO TARAJIWA KUHIT SANA

JULIAS NYAISANGA AFARIKI DUNIA "MUNGU AIWEKE ROHO YAKE MAHALA PEMA PEPONI"   AMIN
 Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari mkoa wa Morogoro,Aziz Msuya Amethibitisha  kwa njia ya simu toka mjini morogoro kuwa mtangazaji mkongwe nchini Tanzania Julius Nyaisanga 'Uncle J" amefariki dunia  leo asubuhi katika hospitali ya Mazimbu iliyoko katika Chuo cha Sokoine cha Kilimo (SUA) eneo la Mazimbu alikokuwa amelazwa.
Msuya ameeleza kuwa Mwili wa Marehemu utahamishiwa katika hospitali ya mkoa wa Morogoro asubuhi hii kwa ajili ya taratibu zingine.
Nyaisanga alikuwa ameshaomba likizo ya mapumziko kutokana na kutoka Radio Aboud ambako alikuwa akifanyakazi kutokana na kuugua



Kwa mujibu wa chanzo chetu taarifa za kifo chake zimezagaa asubuhi hii na bado haijafahamika zaidi sababu za kifo chake



Julius Nyaisanga  alijulikana sana tangu akifanya kazi Redio Tanzania sasa hivi inajulikana kama TBC Taifa,ITV na Redio One stereo kabla ya kwenda Morogoro kujiunga na Radio Aboud.


Saturday, 19 October 2013

YANGA VS SIMBA 20TH OCTOBER 2013

HIVI NDIVYO VIKOSI VYA SIMBA NA YANGA VITAKAVYO ZAMA DIMBANI LEO HII KUSAKA POINT TATU MUHIMU...



LANGONI…
Akianza Andrew Ntalla, au Abbel Dhaira kwa upande wa Simba SC, yeyote bado lango la Wekundu wa Msimbazi litakuwa kwenye mikono salama.  Kwa wote, hakuna kati yao aliyewahi kudaka timu hizo zikimenyana, lakini kabla ya kujiunga na Simba SC, wote wamekwishadaka dhidi ya Yanga, Ntalla akiwa Kagera Sugar na Dhaira akiwa Express ya kwao, Uganda. 
Lakini kwa kuwa tangu msimu umeanza Mganda, Dhaira ndiye amekuwa akisimama langoni mwa Simba SC, bila shaka kesho ataendelea. Huyu ni kipa mrefu mzuri na hodari wa kucheza krosi na mipira ya juu kwa ujumla na zaidi ana uzoefu wa kimataifa akiwa ameidakia Uganda mechi kubwa za mashindano makubwa- na ikumbukwe alikuja Simba SC akitokea Ulaya, alikuwa anadaka klabu ya Ligi Kuu Iceland, IVB.


 Upande wa Yanga SC, Ally Mustafa ‘Barthez’ bila shaka ataanza na hiyo itakuwa mechi yake ya pili akiwa Jangwani kudaka dhidi ya Simba na ya tatu kwa ujumla katika mapambano ya watani, pamoja na ile aliyodaka akiwa Simba dhidi ya Yanga Aprili 19, mwaka 2009 timu hizo zikitoka 2-2.  Barthez ni kipa mzuri, ingawa siku za karibuni amekuwa akifungwa japo bao moja karibu katika kila mechi, ingawa mara nyingi hutokana na makosa ya mabeki wake. Lakini kwa sababu huu ni mchezo mkubwa, bila shaka Barthez atakuwa makini zaidi kesho akipangwa. Lakini hata ikitokea ‘bahati’ ikamuangukia Deo Munishi ‘Dida’ aliyesajiliwa msimu huu kutoka Azam, hapana shaka naye anaweza kufanya kazi nzuri.

SAFU ZA ULINZI:
Kwa Simba, Chollo bila shaka atacheza kulia, kushoto Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ na katikati Kaze Gilbert na Joseph Owino, wakati kiungo wao mkabaji atakuwa Jonas Mkude au Abdulhalim Humud. Ukiondoa Mkude na Chollo ambaye kwa sasa ndiye Nahodha wa Simba SC, wengine wote katika safu ya ulinzi ya Simba ni wapya- Dhaira alikuwepo tangu Januari lakini hakucheza dhidi ya Yanga Mei mwaka huu na Owino amewahi kucheza Msimbazi msimu wa 2010/2011 baada ya hapo akawa nje kwa maumivu ya goti na alipopona akaenda Azam kwa msimu mmoja kabla ya kurejea kwao Uganda ambako amefufua makali na hatimaye msimu huu amerejea Simba SC. Humud amerejea Simba SC msimu huu baada ya misimu miwili ya kuwa Azam. Ukuta wa Simba SC uko madhubuti, ingawa mechi ya kesho ni kipimo chake kingine, tena kikubwa.
Kwa Yanga, Mbuyu Twite hapana shaka ataanza kulia, kushoto David Luhende, wakati katikati watakuwa Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kevin Yondan, kiungo wao mkabaji, Atjhumani Iddi ‘Chuji’.  Uzuri wa Twite zaidi ni katika kusaidia mashambulizi na kurusha mipira kama anapiga, ila kwenye ukabaji anapokutana na wachezaji wenye kasi na uwezo wa kumiliki mpira aina ya Ramadhani Singano, Twaha Ibrahim ‘Messi’ na Haroun Chanongo huwa uchochoro, lakini Luhende hakuna shaka atakaba vema na kusaidia mashambulizi pia.


 SAFU YA KIUNGO:
Kwa Simba SC, Mkude atacheza chini au Abdulhalim Humud, juu Said Ndemla au Amri Kiemba, pembeni kulia Twaha Ibrahim ‘Messi’ na Chanongo kushoto. Mkude, Humud tayari wote wazoefu wa mechi za watani na hakuna shaka yeyote kati yao ataiunganisha timu vizuri tu pale chini. Tofauti ya Ndemla na Amri Kiemba ni uzoefu tu, lakini kwa uwezo wa kuichezesha timu wote wazuri. Watu wa pembeni, Chanongo na Twaha wote wana kasi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira, kupiga chenga na kukimbiza, kupangua ngome. Wote wanaweza kufunga ingawa uzoefu unamfanya Chanongo awe zaidi ya Twaha. Ni matarajio Simba leo itashambulia zaidi kutokea pembeni. Mabeki wa Yanga watakuwa na kazi. Lakini pia kuna hatari makocha wa Simba wanaweza kujichanganya katika uteuzi wa kikosi cha kwanza, kwa sababu timu hiyo imesheheni viungo na mawinga wengi.       
Upande wa Yanga SC, Chuji atacheza chini, juu yake Frank Domayo, kulia Mrisho Ngassa na kushoto Haruna Niyonzima. Hakuna shaka juu ya Chuji pale chini na zaidi zile pasi zake ndefu kwa watu wa pembeni huzalisha mashambulizi vizuri sana. Domayo ni starehe tu kwa wana Yanga pale mbele na pembeni nako Ngassa ‘kama unanawa’, wakati Niyonzima japo hana kasi ya kulinganisha na mwenzake, lakini ni mtu anayefanya vitu vya uhakika. Ngassa kasi zaidi na Niyonzima uwezo mkubwa wa kumiliki mpira, wote wanapangua ngome, wanapiga chenga na kufunga. Dhahiri mabeki wa Simba watakuwa na kibarua kizito kesho na kwa Niyonzima na Chollo yatakuwa marudio, ila Baba Ubaya na Ngassa ni picha mpya


SAFU YA USHAMBULIAJI: 
Kwa Simba Simba SC bila shaka Betram Mombeki ataanza pamoja na Amisi Tambwe. Hii ndiyo mechi ambayo Mombeki na Tambwe wanaweza kutengeneza heshima na si kwa kuwafunga Mgambo JKT. Mombeki ana uwezo wa kucheza mpira, nguvu na anaweza kufunga pia. Anakosa uzoefu tu wa mechi za watani kama mwenzake Tambwe. Lakini kama atatulia, kwa umbo lake na nguvu zake, amini Cannavaro na Yondan watalala na viatu. Upande wa pili, mtaalamu Tambwe yeye atakuwa anasoma tu pilika za Mombeki na mabeki wa Yanga kusubiri mpira utapotelea wapi, auwahi kuutumbukiza nyavuni. Tambwe ni mjanja sana na bila shaka kesho atakuwa mjanja zaidi, kwa sababu amekwishaambiwa kuhusu mechi za watani.
Kwa Yanga, ni Didier Kavumbangu na Hamisi Kiiza ndiyo wataanza kwa sababu ndiyo ambao wamekuwa wakicheza pamoja siku za karibuni. Wawili hawa ndiyo wafungaji wa mabao mawili yaliyopita Yanga SC ushindi wa 2-0 katika mchezo uliopita wa watani. Hizi mbili ni mashine na kwa hakika Kaze Gilbert na Owino wanatakiwa kufanya kazi haswa na si mzaha, vinginevyo watafuata nyayo za akina za Paschal Ochieng na Komabil Keita kuonyeshwa mlango wa kutokea Simba SC



 BENCHI;
Upande wa Simba SC, mbali na kocha Mkuu, Abdallah Kibadeni, msaidizi wake Jamhuri Kihwelo, kocha wa makipa James Kisaka, Meneja Nico Nyagawa na Dk Yassin Gembe, watakakuwepo Ntalla, Haruna Shamte, Adeyoum Ahmed, Hassan Isihaka, Humud, Ndemla, Ramadhani Singano, Sino Augustino, Edward Christopher, Rashid Ismail, Zahor Pazi na Marcel Kaheza. Abdallah Seseme hajaonekana kwa muda mrefu. Kuna uwezekano Kibadeni akawainua Singano na Edward kuongeza nguvu ya mashambulizi kipindi cha pili, ingawa Zahor Pazi ni mzuri zaidi, lakini damu yake haijaendana na makocha hao wote.  
Kwa Yanga SC, mbali na kocha mkuu Mholanzi, Ernie Brandts, Msaidizi wake, Freddy Felix Minziro, kocha wa makipa Razack Ssiwa, Dk. Nassor Matuzya na Meneja Hafidh Saleh, watakuwepo Dida, Juma Abdul, Oscar Joshua, Rajab Zahir, Job brahim, Salum Telela, Hamisi Thabit, Abdallah Mguhi, Nizar Khalfan, Simon Msuva, Shaaban Kondo, Jerry Tegete, Hussein Javu na Said Bahanuzi.
Nizar ama, Msuva au wote na ama mmoja au wawili kati ya Tegete, Bahanuzi na Javu wanaweza kuchukua nafasi za watu kipindi cha pili.
Pamoja na ubora wa wachezaji, lakini mifumo na falsafa za uchezaji zitachangia sana matokeo katika mchezo wa kesho. Tumejionea katika mechi za karibuni, timu zote zinaweka mpira chini, unapitishwa kwenye njia zake mabao yanatafutwa kwa utengenezaji wa nafasi. Tumekwishatoka kwenye Simba na Yanga za enzi zile, ‘hakuna kuremba’ na sasa soka inachezwa.  Tunasubiri kuona makocha, mzalendo wa Simba SC, King Kibadeni na Mholanzi wa Yanga SC, Ernie Brandts wametuandalia nini siku ya kesho. Zaidi ya hapo, marefa tu wazingatie sheria 17 na wawe makini, mtu afungwe kihalali akalie na wachezaji wake. For the good of the game. Fair play.  

 

ADAM JUMA AANDAA FILAMU MPYA ITAKAYO JULIKANA KAMA "PROTOCAL AGENT OF DEATH"

ADAM JUMA wa NEXT LEVEL au VISUAL LAB  alikuwa chimbo kuandaa booonge la filamu itakayoitwa  PROTOCAL AGENT OF DEATH ambayo itaingia mtaani hivi karibuni......stay tunned 
Hii ni zaidi ya NEXT LEVEL

HIVI NDIVYO ITAKAVYO KUWA

Monday, 14 October 2013

KIJANA ALIYE FANANA SANA NA KUNUMBA (MAZIWA KWA TUI LA NAZI)


Unaweza kuKijana aliye fanana sana na kanumba aonekana katika kipindi cha Uswazi kinacho rushwa kila siku ya jumapili katika kituo cha television cha East Africa television....KAMA INAVYO ONEKANA KATIKA PICHA HAPO JUU

Saturday, 12 October 2013

PATA IPAD NZURI NA YAKISASA KWA BEI RAHISI ......TUNAZO ZA 4GB NA 8GB....KWA MAWASILIANO PIGA NAMBA 0653830825

Breaking News
Loading...

Search This Blog

LIKE PAGE ZETU ZA FACE BOOK

ZINGINE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...