MICHONGO KAMILI

Saturday, 26 April 2014

SHEREHE ZA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR ZAFANA.




Sherehe za muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilizo fanyika katika uwanja wa zamani wa taifa zimefana sana kwa halaiki na maonyesho ya kijeshi yaliyofanywa kuanzia asubuhi hadi mchana huku mgeni rasmi akiwa raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania, sherehe hizo zimefanyika huku mwenyekiti wa bunge maalum la katiba akiwa ameahirisha shughuri za bunge hilo ili kupisha bunge la kujadili bajet liendelee na shughuli hiyo hadi mwezi wa nane ndio bunge maalum la katiba litaendelea.

Tuesday, 22 April 2014

HATIMAYA MOYESA ATUPIWA VIRAGO

 

Mkufunzi mkuu na meneja wa klabu ya Manchester United David Moyes ametimuliwa.

David Moyes amefutwa kazi baada ya kushikilia usukuni wa klabu hiyo kwa miezi kumi tu.

Moyes, mwenye umri wa miaka 50, aliteuliwa na Ferguson kumrithi alipostaafu mwaka jana baada ya kuwa na klabu hiyo kwa miaka 26.

Taarifa kutoka kwa klabu hiyo imemshukuru Moyes kwa bidii, uaminifu na hekima aliyoonyesha kocha huyo akiwa mkufunzi wa Manchester United.

Moyes alichukuwa usukani wa kuifunza Manchester United mwaka uliopita baada ya aliyekuwa kocha wa siku nyingi Sir. Alex Ferguson kustaafu.

Huku zikiwa zimesalia mechi nne pekee msimu wa ligi kukamilika Mancheseter united inashikilia nafasi ya saba kwenye jedwali la msimamo wa ligi hiyo alama ishirini na tatu nyuma ya viongozi Liverpool.

Klabu hiyo imeshindwa kufuzu kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa ulaya kwa mara ya kwanza katika kipindi cha takriban miaka ishirini.

NI KIJANA MWENYE UMRI USIO ZIDI MIAKA 25 ALIYE SOMA ALFAROUQ SEMINARY AKAENDA LIDA BOYS ILIYOPO LINDI NA SASA YUPO CHUO FLANI FLANI HIVI AKIWA NA KIPAJI CHA AJABUUUU ALIANZIA KUPAZA SAUTI CHINI YA MITI ALIPO KUWA LIDA BOYS LAKINI ALIPO FIKA CHUO ALIKUTANA NA PRODUCER AITWAE CHRISS NA AKAMPA NAFASI YA KUPAZA SAUTI MBELE YA KIPAZA NA HII NGOMA HAPO CHINI NDICHO KILICHOJIRI.............PERFECT FOR BEGGINER! NAIDEDIKET HII KWA WAPENZI WA BLOG HII .....I MISS YOU SO MUCH



Sunday, 13 April 2014

ALAZWE MAALI PEMA PEPONI REJENDARI MAALIM GURUMO




inna lilah wainna ilaih rajiun...Ni mzee wa siku nyingi sana kwenye
muziki Tanzania ambae aliwahi
kuingia kwenye vichwa vya habari
mara nyingi hasa kutokana na
kuugua kwake kuliko mfanya asitaafu
kabla ya kuzawadiwa gari na
mwanamziki wa kizazi kipya
“Nasibu” au Diamond
Taarifa zilizothibitishwa na hospitali
ya Taifa Muhimbili  zimesema Mzee huyu
amefariki dunia akiwa hospitalini
hapo leo April 13 2014 saa nane
mchana baada ya kupelekwa  jana
asubuhi na kulazwa kwenye wodi
namba 6 ya Mwaisela kutokana na
kuzidiwa.
Tayari mwili wake umepelekwa
kwenye chumba cha kuhifadhia maiti
msiba upo nyumbani kwa marehemu Tabata makuburi
na mimbango ya mazishi itafanyika hapo.
Blog hii inatoa pole kwa wafiwa wote na
wapenzi wa muziki mzuri uliokuwa ukifanywa na
mzee wetu Maalim gurumo
MUNGU AILAZE MAHALI PEMA
PEPONI ROHO YA MAREHEMU
MAALIM GURUMO
“AMIN"

Friday, 4 April 2014

HII NDIO HOTUBA YA RAIS KIKWETE BUNGE LA KATIBA MARCH 21 2014 BUNGENI DODOMA

Kwanza kabisa nianze kwa kuwaomba radhi kwa kuchelewa kuwawekea kitu muhimu kama hichi, hii ni hotuba ya muheshiwa rais JK akihutubia bunge maalum la katiba mjini dodoma mwezi march tarehe 21  2014 . unaweza kudownload  audio  yake  hata video yake pia ilikuweza kufuatilia kilichoendelea siku hiyo....nime fanya hivi ili kuwapa wasomaji wangu nafasi ya kuwa na audio ya hotuba hii kwaajili ya kufuatilia zaidi juu ya kinachoendelea mjini dodoma...




 

MICHONGOKAMILI.BLOGSPOT.COM

KATANGAZEEE NI HII HAPAAA (DOWNLOAD HAPA)


Wednesday, 2 April 2014

TRENI YA MWAKYEMBE INATUTIA MASHAKA!!!!

 

 Ni kama mwaka mmoja na nusu sasa toka treni ya shirika la reli la tanzania (TRL) ianze kufanya safari zake za kusafilisha abiria kupitia maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam, treni hii imekuwa msaada mkubwa kwa watu wanao tokea maeneo yenye idadi kubwa ya wakazi wa jiji hili ambamo treni hiyo imekuwa ikipiga ruti zake za kila siku ukiacha mbagara, kama wewe ni mmoja wa watumia wazuri wa treni hiyo utakuwa umeshuhudia idadi kubwa ya watu wanaotumia usafiri na kupunguza foleni kubwa zilizokuwa zikitokea maeneo ya posta,kariakoo na buguruni


treni hii imekuwa ikikumbwa na matatizo kadhaa ambayo kwa jicho la pili yanaonekana yanazuilika kama ilivyo pata ajari ya kugongwa na roli lenye namba za usajili T 124 ATG   mnamo tarehe 03 October mwaka 2013 lakini tatizo hili lisingewezakutokea kama askari wa barabarani wange tumika maeneo ambayo treni hiyo inapita ikikatiza katika barabara mama za jiji zinazo pitisha magari kwa wingi zaidi kama ile ya buguruni,tabata na ubungo, lakini kikubwa kilicho igusa blog hii hadi kuandika juu ya usafiri huu ni usumbufu uliotokea siku mbili mfululizo kati ya tarehe 1 hadi 2 ya mwezi wa 4 mwaka huu 2014, tarehe 1 mida ya usiku wa saa mbili treni hiyo ilitakiwa imalizie safari yake ya mwisho kutoka stesheni hadi ubungo, abiria wake walikata tiketi kama kawida na kuingia kwenye treni hiyo tayari kwa kysafiri lakini ilipofika saa 2 na dakika kama 20 hivi ilitangazwa kuwa treni hiyo haitoweza kumalizia safari hiyo na abiria wanaombwa radhi kwa usumbufu huo, tatizo kubwa lililotajwa ilikuwa kufeli kwa injini zinazo sukuma gari moshi hilo lakini ilipofika tarehe mbili tena mwandishi wa blog hii alifika katika stesheni hiyo ili kujua kama treni hiyo imeanza safari zake au la! lakini alikuta milango ya ofisi hizo imefungwa na hakuna tangazo lolote lililowekwa kuwataarifu abiria wa usafiri huo ambao jana yake walikatishwa tiketi na hawakurudishiwa pesa zao kwa madhumuni ya kutumia usafiri huo kesho yake yaani tarehe 2 . hivi ni kweli TRL inakosa pesa ya kufanya matengenezo ya injini za treni hizo? kwa mahesabu ya haraka haraka kama kila abiria mmoja analipia shs 400 kwa safari moja na treni ni hiyo kwa kadilio la chini ina uwezo wa kuchukua takribani abiria 1000, hii inaleta jumla ya shs 400000 kwa safari moja tu! chakujiuliza ni  je kwa siku inafanya safari ngapi? na inaingiza shilingi ngapi? na ina muda gani toka ianze! hadi shirika hilo likose pesa ya kufanya marekebisho ya injini hizo?. mi sina mengi yakunena! ni hayo tu!!!
MICHONGOKAMILI.BLOGSPOT.COM

Thursday, 27 March 2014

HATIMAYE MABAKI YA MALAYSIA AIR LINE YAPATIKANA KUSINI MWA BAHARI YA HINDI

VIDEO IKIMUONYESHA BWANA HISHAMMUDIN HUSSEIN AKITOA UFAFANUZI



Nisiku ishirini sasa tokea ndege ya Malaysia air line ipotee na msako mkali umekuwa ukiendelea katika fukwe za china na Malaysia ambako ndipo ndege hiyo ilipokuwa ikihofiwa kupotelea. Hivi karibuni satelaiti za Australia ilipata picha inayo onyesha vipande viwili vinavyosadikika kuwa ni vipande vya mabaki ya ndege hiyo inayo hisia kuwa imepata ajari kataka fukwe hizo, mapema baadae satelaiti za china nazo zili ripoti kuwa zime pata picha inayo onyesha kipande kimoja kikielea karibu na fukwe za china upande wa bahari ya hindi.
Lakini juma tano ya tarehe 26 waziri wa ulinzi wa Malaysia bwana Hishammuddin Hussein aliwaita waandisha wa habari na kuwambia kuwa satelait za ufaransa nazo zilitoa taarifa iliyoambatana na picha ikionyesha vipande 112 vilivyo karibiana vikielea katika bahari ya hindi upande wa kusini, vipande hivyo vikiwa vimeachana kwa umbalai wa yadi 25 kutoka kimoja hadi kingine bwana Hishammuddin Hussein aliongezea kwakusema kuna vingine vilionekana viking’aa sana nah ii inaashiria ni vitu vigumu kama mabati au plastiki,picha hizo zilipigwa na kampuni hiyo ya kifaransa siku ya jumapili kwa kutumia satelaiti 5 zilizokusanywa pamoja ilikufanya zoezi hilo. hii imekuwa ni dalili kubwa zaidi kuliko dalili zote zilizowahi kutokea kuhusiana na uwezekano wa ndege hiyo kuwa ilipata ajari katika bahari ya hindi, nduga na jamaa waliokuwa na ndugu katika ndege hiyo wame kataa kabisa ushahidi huo na wameandamana katika miji ya china na Malaysia wakitaka kutafutwa kwa “BLACK BOX” kifaa kinacho tunza kumbukumbu kuhusiana na matukio yote yaliyokuwa yakiipata ndege hiyo, japo kuwa ianahisiwa kuwa kifaa hicho huenda kilipata hitilafu katika “power source” yani chanzo chake cha nishati au kuishiwa na betri na kushindwa kufanya mawasiliano na kupelekea ndege hiyo kupotea kwanye rada mara kabla ya kudondoka katika bahari Ya hindi. na Kwa upande wa pili serikeli za china,Malaysia,marekani na japan zimepeleka vikosi vyao katika eneo hilo,

Wanamahesabu wana kadiria kuwa ndege hiyo inawezekana ikawa imedondoka maili 1,500 kutoka katika fukwe za Australia hivyo hii imepelekea kupunguzwa kwa uneo la uchunguzi hadi karibu na eneo hilo lililopo karibu na fukwe hizo za Australia..NI HAYO TU!!
MICHONGOKAMILI.BLOGSPOT.COM

Monday, 24 March 2014

SHILOLE AJA TENA NA NGOMA MPYA - CHUMABUZI

KWA MUJI WA SHISHI YAANI SHILOLE ANASEMA NGOMA HII AMETOA ISIPIGWE KWENYE TV STESHENI KWASABABU NI "EXPLICITY VERSION" KWA WENYE MIAKA 18 NA KUENDELEA TU!!!!!!  NA MKAE TAYARI KWA VIDEO YA KURUSHWA KWENE MEDIA.
MICHONGOKAMILI.BLOGSPOT.COM

Friday, 21 March 2014

ITS THE HOTTEST UEFA QUATER FINALS ONCE AGAIN 2014 IN LISBON



European champions Bayern Munich will play Manchester United in the Champions League quarterfinals.

WAKICHAGUA TIMU - VIDEO
...........
GettyImagesMoyes will face Guardiola's all-conquering Bayern in his first ever Champions League quarterfinal.
Bayern dispatched Arsenal in the last-16 and will now seek to beat United, whom they defeated at this stage of the competition en route to the final in the 2009-10 season. United, victors against Bayern in the 1999 final, will have to spring an upset to keep alive any hope of major silverware in David Moyes’ debut season.
Bayern sporting director Matthias Sammer warned his players not to be complacent despite United’s disappointing form.
“In the last 16 return leg, they showed they are capable of great things. On good days, they are extremely dangerous,” he said on the club’s official Twitter account. “We must not allow them to have two good days. I think the draw is doable, but also dangerous.”
We've met @FCBayern nine times before in Europe, winning two games, drawing four and losing three. #MUFCBAYERN
— Manchester United (@ManUtd) March 21, 2014
Real Madrid, meanwhile, will look to make amends for their defeat to Borussia Dortmund in the semifinals of last year’s competition as they attempt to maintain their charge towards a long-awaited 10th European crown.
Dortmund CEO Aki Watzke said the draw was unfortunate for his team, who had also played Madrid in the group stage last season.
“There was no easy draw, but it’s not that nice that we have to play them for the third time in 18 months,” he said. “We are rank outsiders. It’s the same [Madrid] team, really. They’ve swapped [Gareth] Bale for [Mesut] Ozil but Real, alongside Bayern Munich, are the best team in Europe right now. It’s very difficult task indeed.”
Dortmund, who have endured severe injury problems this season, will also be without star striker Robert Lewandowski for the game at the Bernabeu after he was controversially booked in the last round against Zenit St Petersburg.
“Lewandowski’s absence in the first leg is bitter, even more so because it was a laughable decision,” Watzke added. “Real have a lot of respect for Lewandowski.”
 this news is in respsct of CHAMPIONSLEAGUE.COM
MICHONGOKAMILI.BLOGSPOT.COM

Wednesday, 19 March 2014

Unanichora - Ben Pol & Fundi Samweli

MISTARI YA MTANZA HURU YASUMBUA VICHWA VYA MAKACHERO


Jina halisi anaitwa babuu nixt akiwa anatumia jina la kisanii “b.o.t” aliamua kuingia studio inayo julikana kwa jina la “5records” kufanya nyimbo inayokwenda kwa jina la MTANZA  HURU  huku akimshirikisha staa flani hivi wa mzikihapa bongo lakini kutokana na mistari iliyopo katika nyimbo hii msanii huyo

alishikiliwa na askari na ikabidi mmiliki wa nyimbo yani B.O.T aitwe nakuyazungumza na askari hao lakini kupitia msaada wa mwanasheria flani hivimchongo ukawa umemalizwa kisheria lakini bado staa huyo aliye shirikishwa aliomba kipande chake kitolewe...na kama ilivyo ada B.O.T akajaribu kumtafuta mtu mwingine wa kuziba pengo hilo ndipo alipopatikana fundi SUPER ZEE na kuziba pengo hilo na kuiachia ngoma hii isumbue TZ, Ngoma yenyewe ni hii hapa chini.

Friday, 14 March 2014

KUPOTEA KWA NDEGE YA MALAYSIA AIR LINE BADO NI KITENDAWILI


Ni takribani siku 7 sasa tangu ndege ya Malaysia air line ipotelee kusiko julikana mara baada ya kutoweka ghafla kwenye rada za vituo vya usimamizi wa  mambo ya anga vya Malaysia, ilipotea wakati ikiwa katika anga hewa la mashariki mwa fukwe za Malaysia au kusini mwa fukwe za china,

 ndege hiyo yenye namba MH370 ilipotea siku ya jumamosi ya tarehe 9 mwezi wa 3 mwaka huu 2014, ilipotea ikiwa na abiria 227 na wafanya kazi 12 kati ya abiria hao, kwa mujibu wa bwana Ronald Kenneth Noble ambaye ni   Interpol Secretary General, inasemekana kuna abiria wawili amabao walikuwa wakisafili ndani ya ndege hiyo kwa kutumia paspoti feki au za kugushi, hii imezua wazo kwa watafiti wa mambo kuwa kuna uwezekano ndege hiyo ikawa imetekwa na magaidi kwaajili ya kuitumia katika shughuri zao za kigaidi, hawa hapa chini ni abiria hao wawili wanao dhaniwa kuhusika na upotevu wa ndege hiyo kama walivyo tajwa na bwana  Ronald Kenneth Noble, japokuwa hakuna mwenye uhakika juu ya hilo hadi sasa.
Ni siku sita sasa tangu kupotea kwa ndege hiyo na serekali  za Malaysia na china zikishirikiana na serekali ya marekani zimekuwa zikifanya jitihada za kutafuta alama yoyote itakayoweza kuwaonyesha wapi ilipo ndege hiyo,

 inasemekana hadi serekali ya Malaysia ikaamua kutumia na waganga wa jadi ambao ni maarufu katika hiyo kama mganga huyu maarufu anaye itwa bwana Ibrahim Mat Zin
Siku mbili baada ya kupotea kwa ndege hiyo ilizuka habari kuwa kuna abiria wa ndege nyingine ameweza kupiga picha usiku kupitia dirishani ikionyesha cheche za moto katika uso wa bahari ya kusini mashariki mwa bara la asia na inawezekana ikawa ni Malaysia airline imedondoka katika usawa wa bahari na kuripuka moto lakini hii nayo ikabaki kuwa moja ya uzushi tu mara baada ya vikosi vya uokoaji kutembelea eneo hilo na kukuta hakuna chochote Zaidi ya meli na boti kadhaa,
Nadharia mbalimbali zinaendelea kutolewa na watu mbalimbali juu ya ilipo ndege hiyo, wengine wanasema inawezekana ikawa ni pembe ya Bermuda ambayo haipo katika ramani ya dunia, Bermuda ni maarufu kwa upotevu wa ndege na meli nyingi Zaidi duniani  pembe tatu hiyo inaundwa na  miji ya  Miami,San juan,PUERTO Rico pamoja na Bermuda yenyewe meli na ndege nyingi zilizopotelea humu zilipotea kwanza kwenye rada za control towers na baadae hazikupatikana hadi leo na hicho ndicho kinachowapa wasiwasi watu wanao isapoti nadharia hii,

 lakini nadharia hii imekosa nguvu baada ya kugundulika kuwa  maeneo hayo ndio maeneo yanayo ongoza duniani kwa kuwa na safari nyingi za majini na angani kwahivyo upoteaji wa vyombo hivyo unaweza kuwa ni kwa bahati mbaya tu! Na hivyo hakuna uhusiano wowote kati ya upoteaji wa ndege hiyo na pembe tatu ya Bermuda.
Nadharia nyingi zimekuwa zikitolewa ikiwemo ya kuvihusisha viumbe kutoka sayari nyingine na upoteaji kwani rada za kijeshi zilinasa kifaa cha umeme kilichosemekana kupita karibu na njia ya ndege hivyo kwa kasi ya kutoweza kunaswa na kamera za rada hizo,lakini hii pia imekosa ushahidi wakutosha .
Pamoja na nadhari zote hizo lakini bado ndege hiyo haijulikani ilipo hivyo wananchi wenye ndugu waliokuwa kwenye ndege hiyo wanamuomba mungu ndege hiyo ipatikane kama inavyoonekana hapa chini maelfu ya waislamu wa Malaysia wakiswali sala ya kuiombea ndege hiyo ipatikane
Na wakati huo huo vikosi vya uokoaji vya Malaysia,China na Marekani vikiendelea kupanua  maeneo ya utafutaji hadi maeneo ya Malacca.

macho ya ndugu hao yamejaa machozi na sura zao ni zenye huzuni kwa asilimia mia moja..


MUNGU SAIDIA KUPATIKANA KWA MH370
MICHONGOKAMILI.BLOGSPOT.COM
Breaking News
Loading...

Search This Blog

LIKE PAGE ZETU ZA FACE BOOK

ZINGINE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...