MICHONGO KAMILI

Saturday 7 June 2014

INASEMEKANA ULE UTATA KATI YA MALAWI NA TANZANIA UMEAMKA UPYAAA



RAIS MPYA WA MALAWI AITANGAZIA TANZANIA VITA
RAIS mpya wa Malawi Profesa Peter Mutharika
ametangaza vita na Serikali ya Tanzania,mara tu
baada ya kuapishwa. Akizungumza na Mwandishi
wa Habarimpya.com nchini Malawi baada ya
sherehe za kuapishwa kwake kuhusu kauli yake
aliyoitoa mwaka jana wakati akiajiandaa na
kampeni za uchaguzi mkuu kwamba suala la Ziwa
Nyasa haliwezi kuchukua nafasi katika serikali yake
kwakuwa ziwa ni mali ya Malawi.
"Siwezi kusema chochote kwa sasa kuhusu suala
la Ziwa Nyasa kwa sababu nilisha toa msimamo
wangu hivyo kilicho baki ni utekelezaji"alisema
Rais Mutharika kwa ufupi.
mapema mwaka jana Mutharika alisema kwamba,
nchi zote mbili yaani Tanzania na Malawi hazina
cha kujadili kuhusu suala la Ziwa Nyasa (Ziwa
Malawi) kwa sababu hilo Ziwa ni mali ya Malawi.
Akiwa katika mkutano wa siasa mjini Chipoka
nchini Malawi August 3 2013 Mutharika alisema
kwamba,"Hakuna haja ya kujadili suala la Ziwa
Malawi kwakuwa ni mali ya Malawi na itaendelea
kuwa mali yetu, tutakapo chukua nchini mwakani
ujinga huu wote utamalizika kwa sababu hivi sasa
Tanzania inajigamba kwa sababu Serikali
inaongozwa na viongozi wajinga"alisema Mutharika
na kuongeza:.
"Nitaongeza meli nyingi za uvuvi na usafirishaji
katika ziwa hilo kwa ajili ya kuinua uchumi wa nchi
na ajira kwa vijana wa Malawi, hili litawezekana
kwa sababu Tanzania haina hata inchi moja ya
umiliki wa Ziwa hilo".
Wakati wa utawala wa Rais Joyce Banda Serikali
yake likuwa katika mgogoro na Serikali ya
Tanzania kuhusiana na umiliki wa Ziwa hilo, huku
akitangaza kwamba yuko tayari kupigana vita na
Tanzania ili kuilinda Ziwa hilo lenye utajiri mkubwa
wa mafuta.
Hata hivyo Uchunguzi uliofanywa na Mwandishi wa
Habarimpya.com nchini Malawi imebaini kwamba
kati ya mambo yaliyo mpa Mutharika ushindi ni
pamoja na ahadi yake kwa wananchi kuhusu Ziwa
Nyasa.
Malawi na Tanzania tayari zimewasilisha ushahidi
na majibu ya maswali kuhusu umiliki wa maeneo
kwenye Ziwa Nyasa, kwa jopo la wasuluhishi
linaloongozwa na Rais mstaafu wa Msumbiji
Joachim Chissano.
Wasuluhishi hao walizitaka Malawi na Tanzania
kutoa majibu ya maswali manne muhimu, wakati
wakiwasilisha ushahidi wao kuhusu umiliki wa ziwa
hilo wenye mgogoro. Mgogoro huo uliibuka baada
ya Serikali ya Malawi bila kushauriana na Tanzania
kutoa leseni kwa kampuni mbili za kigeni, kutafuta
mafuta katika eneo la ziwa ambalo linamilikiwa na tanzania Viongozi wa juu wa usalama wa Taifa wamewaomba wanaichi wanaendelea kufanya mazoezi binafsi hata ndani ya vyumba vyao kwaajili ya Kupambana na nduli Prof Mutharika.
Pushapu zinashauriwa zaid kwa ajili ya kuongeza pumzi..

Kuna wasiwas vijana wa vyuo kikuu kupewa kipaumbele zaid kwa ajil ya kutetea nchi yao. Hivyo take your private time to prepare for the war.

HUO NDO MCHONGO WA LEO
Breaking News
Loading...

Search This Blog

LIKE PAGE ZETU ZA FACE BOOK

ZINGINE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...