MICHONGO KAMILI

Thursday 27 March 2014

HATIMAYE MABAKI YA MALAYSIA AIR LINE YAPATIKANA KUSINI MWA BAHARI YA HINDI

VIDEO IKIMUONYESHA BWANA HISHAMMUDIN HUSSEIN AKITOA UFAFANUZI



Nisiku ishirini sasa tokea ndege ya Malaysia air line ipotee na msako mkali umekuwa ukiendelea katika fukwe za china na Malaysia ambako ndipo ndege hiyo ilipokuwa ikihofiwa kupotelea. Hivi karibuni satelaiti za Australia ilipata picha inayo onyesha vipande viwili vinavyosadikika kuwa ni vipande vya mabaki ya ndege hiyo inayo hisia kuwa imepata ajari kataka fukwe hizo, mapema baadae satelaiti za china nazo zili ripoti kuwa zime pata picha inayo onyesha kipande kimoja kikielea karibu na fukwe za china upande wa bahari ya hindi.
Lakini juma tano ya tarehe 26 waziri wa ulinzi wa Malaysia bwana Hishammuddin Hussein aliwaita waandisha wa habari na kuwambia kuwa satelait za ufaransa nazo zilitoa taarifa iliyoambatana na picha ikionyesha vipande 112 vilivyo karibiana vikielea katika bahari ya hindi upande wa kusini, vipande hivyo vikiwa vimeachana kwa umbalai wa yadi 25 kutoka kimoja hadi kingine bwana Hishammuddin Hussein aliongezea kwakusema kuna vingine vilionekana viking’aa sana nah ii inaashiria ni vitu vigumu kama mabati au plastiki,picha hizo zilipigwa na kampuni hiyo ya kifaransa siku ya jumapili kwa kutumia satelaiti 5 zilizokusanywa pamoja ilikufanya zoezi hilo. hii imekuwa ni dalili kubwa zaidi kuliko dalili zote zilizowahi kutokea kuhusiana na uwezekano wa ndege hiyo kuwa ilipata ajari katika bahari ya hindi, nduga na jamaa waliokuwa na ndugu katika ndege hiyo wame kataa kabisa ushahidi huo na wameandamana katika miji ya china na Malaysia wakitaka kutafutwa kwa “BLACK BOX” kifaa kinacho tunza kumbukumbu kuhusiana na matukio yote yaliyokuwa yakiipata ndege hiyo, japo kuwa ianahisiwa kuwa kifaa hicho huenda kilipata hitilafu katika “power source” yani chanzo chake cha nishati au kuishiwa na betri na kushindwa kufanya mawasiliano na kupelekea ndege hiyo kupotea kwanye rada mara kabla ya kudondoka katika bahari Ya hindi. na Kwa upande wa pili serikeli za china,Malaysia,marekani na japan zimepeleka vikosi vyao katika eneo hilo,

Wanamahesabu wana kadiria kuwa ndege hiyo inawezekana ikawa imedondoka maili 1,500 kutoka katika fukwe za Australia hivyo hii imepelekea kupunguzwa kwa uneo la uchunguzi hadi karibu na eneo hilo lililopo karibu na fukwe hizo za Australia..NI HAYO TU!!
MICHONGOKAMILI.BLOGSPOT.COM

No comments:

Post a Comment

0653830825

Breaking News
Loading...

Search This Blog

LIKE PAGE ZETU ZA FACE BOOK

ZINGINE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...