Ni wakati mechi kati ya yanga na al ahly ya egypt ikiendelea mida ya saa 2:30 usiku wa jumapili hii ambapo gari aina ya FUNCARGO yenye plate number T763 AXJ ikiendeshwa na mwanamama ambaye jina lake halikupatikana ilipogonga ukuta wa nyumba iliyopo karibu na ZAHANATI ya kiserekali ya segerea ugombolwa kwa maelezo ya walioshuhudia ajari hiyo inasemekana mama huyo alikuwa amelewa kiasi flani na alikuwa akitokea barabara ya inayo toka shule ya msingi segerea na alipo fika karibu na kona iliyopo kwenye zahanati hiyo alitakiwa akate ili kuelekea barabara ambayo ingempeleka moja kwa moja hadi kituo cha mabasi cha kwa bibi, ndipo hapo alipo kosea badala ya kukanyaga break akajikuta anaongeza spidi na kugonga nyumba iliyopo mbele yake ambayo ni ya bwana mmoja aliye julikana kwa jina la Mr. Msofe. dakika tano baada ya ajari hiyo watu wengi walijaa eneo la tukio akiwemo Mr. Msofe ambaye ni mmiliki wa nyumba hiyo,alipo jaribu kuhojiwa mama huyo ilishindikana kwani alionekana amechanganyikiwa na asingeweza kutoa maelezo yoyote yakueleweka kwa muda huo na pia alikuwa akilalamika kupatwa na maumivu maeneo ya kichwani..
Maajabu yanaendelea katika misitu mbali mbali duniani kama yale ya mbuga za Africa mashariki ya kuhama kwa makundi makubwa ya wanyama kama nyumbu,tembo na vifaru kutoka nchi moja kwenda nyingine kulingana na mabadiliko ya misimu ya hali ya hewa, mbali na maajabu hayo ambayo wazungu wengi wamekuwa wakitiririka maeneo tofauti tofauti ya Afrika ili kujionea, kuna maajabu mengine yaliyo tokea katika misitu ya AUSTRALIA ambapo Nyoka mkubwa maarufu kama GIANT PYTHON amemmeza Mamba mkubwa mwenye zaidi ya tani 1 baada ya kupambana nae kwa zaidi ya masaa matano....angalia video yake hapo juu.
WhatsApp has suffered an outage just
days after it was bought by Facebook for $19billion (£11.4billion).
hichi ni kichwa cha habari kinachowekwa na mtandao waREUTERSsiku ya tarehe 22 feb 2014
mtandao waWHATSAPPuliogunduliwa na Brian Acton na Jan Koum back Ulinunuliwa na wamiliki wa FACEBOOK kwa dolla billion 19 kabla hauja leta hitlafu kwa zaidi ya masaa matatu siku ya tarehe 22 feb 2014 ambapo watumiaji wa WHATSAPP walishindwa kutuma na kupokea picha na video pamoja na mtandao huo kushindwa kukonekti na servers wa mtandao huo kama ilivyo andikwa na mtandao wa habari wa REUTERS katika tareha hiyo hiyo. bado haijawekwa wazi ni kwanini bwanaMark Zuckerberg ambaye ni mgunduzi na mmiliki wa mtandao wa kijamii wa FACEBOOK aliamua kununua mtandao wa WHATSAPP kwa bei kubwa ambayo FACEBOOK kamwe haijawahi kuingia gharama kununua mitandao miongine kama-INSTAGRAM kwa dolla billion 1, BRANCH iliyo nunuliwa kwa dolla million 15 na FACE.COM ya israel ilyo nunuliwa kwa dolla million 100 na zingine nyingi kama TAGTILE,SPOOL,SHAREGROOVE
na mingine mingi ipatayo 45
wamiliki wa mtandao wa WHATSAPP waliomba radhi kwa watumiaji wake waliokua wakikadiriwa kufikia milioni 450 duniani kupitia mtandao wa Twitter siku ya juma mosi mida ya saa 7 na dakika 30 mchana mtandao huo uliendelea kusumbua hadi mida ya saa 11 na dakika 48 mchana ambapo WHATSAPP kupitia twitter kwa mara nyingine ikawafahamisha watumiaji wake ambao wana follow kupitia twitter ambao wapo takriban millioni 1 kuwa WHATSAPP sasa iko sawa na wanaweza kuendelea kuitumia kama mwanzo. wataalam kadhaa wamekua wakitoa mawazo yao kuwa inawezekama bwana Mark Zuckerberg ameamua kununua kila mtandao unaoonekana kupata umaarufu na kutaka kuipiku FACEBOOK ili abakie kuwa kinara wa mitandao ya kijamii duniani.....ni hayo tu
Wakati skendo mbalimbali zikiendelea kuwaandama mastaa
mbalimbali akiwemo staa wa muziki wa bongofleva anaye waburuza wenzie kwa
takribani miaka matano kama si manne sasa ambaye ana endelea kutamba na remix
yake mpya MY NUMBER ONE aliyo fanya na mwanamziki anaye kuja kwa kasi aitwaye
DAVIDO kutoka Nigeria
Blog hii imegundua kuwa maisha ya wasanii wakubwa kama huyu
yamekuwa kama kioo kwa mashabiki zao wanao fatilia muziki wao, kutokana na hili
mwana habari wa blog hii akaona ni wakati sasa wakuwa wapasha habari mastaa hao
kajiepusha na skendo mbali mbali kwa kujihusisha kwao kuna pelekea asilimia
kubwa ya wanajamii kupotea kimaadili na badala yake blog hii inawashauri
wasanii hao kujaribu kwa dhati ya mioyo yao kuwa vioo bora vya jamii na
waadhimie kuibadilisha jamii kupitia vibao vyao mbali mbali kama msanii huyu
alivyo faulu kuwateka mashabiki wake kimavazi kama inavyoonekana kwenye picha
mbalimbali …ni hayo tu! Na huu ndio MCHONGO KAMILI wa leo BY
Wakati skendo kadhaa za mastaa zikiendelea kuvuma mitaani kama ile ya kuhusu Mkubwa DIAMOND kumpa mimba mwanadada fulani wa kitaa na ile ya mwana dada WEMA mwana wa SEPETU kusemekana kutoka kimapenzi na mkali wa bongo fleva anaye tamba na ngoma kama BABY na ONE ANDONLY Blog mbali mbali kama ile ya millad ayo na website ya BONGO MOVIES vina andika kuhusu wema kufunguka kuhusu mapenzi yake kwa diamond MCHONGO KAMILI upo hivi!!!
Mwanadada Wema Sepetu ambaye pia aliwahi kuwa Miss
Tanzania 2006 ambaye kwa sasa anaendesha kampuni yake binafsi iitwayo
Endless Fame inayojishughulisha zaidi na utengenezaji wa Filamu
mbalimbali.
Kupitia kipindi cha Leo tena February 28 Wema Sepetu amekubali
kutaja sifa za mwanaume anayempenda kuwa na mvuto kwake,swali
lililoulizwa na Watangazaji wa kipindi hicho ni kuhusu mwanaume wa sifa
gani anayedhani anaweza kuolewa nae ambapo Wema alijibu “Kuolewa sio
shida je huyo mwanaume nampenda,maana naweza kuja kuchumbiwa lakini
nisimpende”
“Mimi nampenda Mwanaume mweusi,wanaume weupe sio kwamba sijawahi kuwa nao lakini nakuwa sina mzuka nao”.
Alipoulizwa kuhusu uhusiano wake na Diamond amekiri kwa
kusema’Kweli niko na Nasib - Diamond na nadhani muda huu kutakua na
utulivu ndani yake,ule utoto tuliokua tunafanya nadhani ulikua utoto na
imekua Power Couple toka mwaka 2010 kwa hiyo tuna ni miaka 4 sasa,kwa
sasa tumeamua kuwa serious’.
Habari kwa Hisani ya Millard Ayo
Wema Sepetu pia kaandamana na Ant Ezekiel kwenye interview ya kipindi hicho kinachorushwa na Clouds Fm. michongokamili.blogspot.com
Yule mkali anaetikisaTasnia nzima ya Bongo Movie ambae ameweza kuwapiku wakali wengine katika
Tasnia hiyo ya Movie kwa hapa nyumbani Tanzania na baadhi tu ya Filamu zake
ambazo ameshaziachia kama vile BOXEERA, EDA, RAMADHANI KAREEM, na kuweza
kufanya poa sana katika soko la hapa nyumbani na hata kimataifa pia.Na si
mwingine bali namzungumzia Ussi Hajji almaaruf kama “FEY au FEYSAL”
Mkali huyo ambaye makao makuu yake kikazi na hata
kifamilia yakiwa visiwani Zanzibar akiwa chini ya kampuni yake inayofahamika
kama Zan Effects. hivi juzi kati bllog hii ilipata fursa ya kuzungumza nae in an
Exclusive Interview iliyo endeshwa na mmoj wa waandishi wa blog hii mr.Ridhione kupitia Hits fm radio 92.5
Lakini mwanzo kabisa tulitaka kufahamu kuhusiana na
lile kosa aliloweza kulifanya katika filamu yake ya mwisho iliyoko sokoni mpaka
hivi sasa “BOXEERA”, pale ambapo alikuwa ndani ya chumba na yeye akicheza kama
verry sensitive Person “mtu mwenye hisia/machachesana” lakini yule jamaa aliingia mule ndani
na kuchukua kitabu pasi na yeye kugundua chochote kile. Alifunguka kwa kusema
“Sisi ni wanadamu na hakuna mwanadamu mkamilifu,
tumezipokea comment za watu vizuri na tumeahidi kuzifanyia kazi kwa sababu watu
wengi sana walinipigia simu na kunambia kuwa inakuwaje wewe kama jini halaf
mtu anakuja na wewe hujahisi hata chochote?? Ni jamabo ambalo haliwezekani
kabisa. Ila ilikuwa ngumu tu kurudi tena location kutokana na mambo kadha wa
kadha. Hivyo naweza kusema kuwa tutajitahidi kuwa makini pia”
Ila alipomuuliza kuhusiana na maandalizi ya Zan
Effects kwa mwaka huu 2014 kuna nini ambacho kinakuja ama nini wanafanya maaana
ni muda mrefu sasa tangu itoke BOXEERA. Alisema kuwa kutokana na ubora wa
kazi zao ambao huambatana na maandalizi mazuri ambayo lazima yachukue muda
kidogo ………
“Ila soon tyu nitaitambulish The Exclusive one
ambayo inakwenda kwa jina la PRINCE WILTH ambayo itatoka katika miezi hii hii
ya hapa mwanzoni. Ijapo katika mwaka huu wa 2014 kuna movie nyingi tu kutokea
Zan Effectsambazo zitatoka ila hiyo
Prince Wilth itakuwa ya mwanzo as an exclusive. Na naweza kusema kuwa hizi ni
movie ambazo zinaleta mapinduzi katika tasnia ya filamu ambapo ndipo kama
tulivyoanza na Boxeera kama walivyoiona. Lakini mi naahidi itakapotoka nahii
Prince Wilth ndipo watakaposaidiki hili”
Jamaa tulipotaka uthibitisho wa hayo mapinduzi kwa
movie hiyo ya Prince Wilth akatutupia kitu cha trailer ya movie hiyo na
kuifanya blog hii kuwa na sababu mia moja za kuandika habari hii yenye ushahi wakutosha.Ila jamaa alimalizia kwa kusema;
“So mi nitaendelea kufanya vitu vitakavyoleta tofauti
katika tasnia ya filamu, na ningeomba sana watu wangu waendelee kuni support
na kazi zangu ili tuweze kufikia pale ambapo tunafikiria kufika.Nawapenda sana
HATIMAYE Shirikisho la
Soka Duniani, FIFA limemuidhinisha mshambuliaji nyota wa kimataifa wa
Uganda, Emmanuel Okwi kuichezea klabu ya Yanga. Kwa mujibu maelezo wa
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka nchini, TFF, Celesine Mwesigwa
amethibitisha kuwa tayari wameshapokea barua kutoka FIFA ikiwahabalisha
kuwa mchezaji huyo ni halali kukipiga Yanga. Mwesingwa amesema suala
Okwi tayari limeshamalizika ila hawezi kulizungumzia zaidi kwasababu
watatuma taarifa kwa vyombo vya habari kwa ufafanuzi zaidi. Januari 22
mwaka huu ikiwa ni siku mbili tu kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Kamati ya Sheria na Hadhi za
Wachezaji ya TFF ilisimamisha usajili wa Okwi kuitumikia Yanga ili
kwanza upatikane ufafanuzi kutoka FIFA juu ya uhalali wake kucheza timu
hiyo. Kamati hiyo ilifikia iliamua hivyo kwasababu ya mgogoro wa
mchezaji huyo na klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia ambapo kulikuwa na
taarifa kuwa alipewa kibali cha muda kuichezea SC Villa ya nchini kwao
ili kulinda kiwango chake.
Yule mshkaji ambaye
alijitahidi kufanya poa sana katika Industry ya Bongo Fleva kwa hits songs zake
kadhaa ikiwemo "Sababu ya Ulofa" na nyinginezo zikiwa zime recordiwa
ndani ya Sharobaro Records chini yake Raisi wa Masharobaro Bob Juniour.
Nadhani kwa intro hiyo si mgeni saaana katika masikio na
macho ya mafuns wa Bongo Fleva a.
He is Top C ambaye kiukweli alipotea muda
mrefu sana katika gemu na kufikia hata kusababisha kuwepo kwa uvumi wa kuwa
jamaa alibahatisha!!! au ndo keshapigwa chini??? na vitu kama hizo
nini..............!!!
TOP
C
Ila juzi kati Top c alifunguka na kuuzima ukimya
wote uliokuwepo dhidi yake na kukanusha suala la kushushwa kimziki na aliyekuwa
bosi wake wa zamani (Babuu Kisouji) alipokuwa chini ya Babuu Entertainment na
Top C kusema kuwa.
"hapana hilo suala si
la kweli, ila tu unajua sisi ni binadamu tunakosea na tunakwazana vilevile.
Kuna mambo tu ya kibinadamu yaliyotokea kati yangu na bosi wangu wa zamani
Babuu Kisouji na hivyo hatukufikia mwisho mzuri ndiyo maana tukaamua kila mmoja
afanye shughuli zake. Ila si kweli kwamba yeye ndiyo kanishusha au kanizuia
nisitoe nyimbo mpya"
Lakini pia Top C alinieleza
kuwa alikuwa na baadhi ya mambo ya kifamilia na nini ndiyo maana akawa kimya,
ila hivi sasa ameshajipanga vizuri na kazi yake mpya ipo tayari na hivi
karibuni tyu itaanzakusikika kwenye
radio stations mbalimbali.
TOP
C NA MAANDALIZI YA KITU KIPYA YAKO HIVIIIIIIIIIIIII
"Kuna baadhi ya vityu
tyu vinamaliziwa na muda mfupi tyu itaanza kusikika katika redio stations
mbalimbali. Sijajua ni lini hasaa itakuwa kwa hewa kutokana na hayo ni masuala
ya management yangu ambayo hivi sasa inanisimamia kazi zangu kutokea kule Kenya
"Canden Kane " Ila ikishakuwa tayari tyu nitaitambulisha"
Na zaidi ya hayo Top C
anawaomba mashabiki wake mumpokee vizuri na mumpe support ya kutosha.
YULE MKALI WA SHKAMOO MZEE NA NYINGINE NYIIINGI YAANI "JB" JACOB STEVENANAKUJA NA CHUMA KINGINE "WAGENI WANGU"
TRAILLER YA WAGENI WANGU
Utakapozungumzia watengenezaji wazuri wa
filamu za Kitanzania huwezi kuacha kuwataja Jerusalem
Film ambayo kampuni hii ipo chini yake Bonge la Bwana “JACOB STEVEN” ambaye pia
katika waigizaji wanaofanya poa sana
hivi sasa katika soko la filamu ndani na nje ya nchi pia huwezi kuacha
kumuorodhesha huyu jamaa.
JB KATIKA POUZI
Juzi kati tulipata fursa ya kuzungumza
nae na tukataka kufahamu mengi sana kutoka kwake
lakini pia kutokea Jerusalem Film akiwa kama mzungumzaji mkuu wa Kampuni hiyo. Na kitu cha mwanzo
kabisa tulichotaka kufahamu ni kuhusiana na suala zima la Jerusalem kutoa
filamu ambazo JB hatujamuona humo ndani hata scene moja, jambo ambalo
limewaumiza vichwa mashabiki wake wengi katika filamu iliyokwenda kwa jina la
BADO NATAFUTA.
alikuwa na haya yakusema;
“Yeah ni kweli, ila lengo la kufanya
hivyo ni kutaka kutengeneza image ya kampuni ya Jerusalem
Film na si lazima ya JB, kwa maana ya kuwa watu wawe na hamu ya kutazama filamu
za Jerusalem. Na
huo naweza nikasema ndiyo mpango wa hivi sasa kwa maana ya kuwa kutakuwa na
filamu za aina mbili ambazo nitakuwa sishiriki na zile ambazo nitakuwa
nashiriki”.
OFFICIAL COVER YA MOVIE AMBAYO IMEFANYA POA SANA 2013 "BADO NATAFUTA"
Lakini jambo jengine ambalo JB
alilizungumzia ni kwamba anawashukuru sana mashabiki wake kwani filamu hiyo ya
BADO NATAFUTA imekuwa filamu ambayo imefanya vizuri sana mwaka jana.Ila bado
tukawa na maswali kwa JB kuwa kwanini ameamua kuhamia katika kutengeneza image ya Kampuni tu na si JB kama JB?
Bi Staa kama anavyojulikana na wengi....
“Hapana, ila unajua jambo muhimu ambalo
tumelilenga hapo ni kuwafanya mashabiki wakishakuwa na imani na Jerusalem ijapo
kuwa JB hayumo ndani ya filamu hiyo itasaidia sana pale ambapo nitakuwa siigizi
tena kutokana na sababu mbalimbali huwenda nimeamua kupumzika, au kwa sababu
nyengine yeyote ile. Hivyo watu bado watakuwa na imani na vitu vinavyozalishwa
na Jerusalem.”
GABO AKIWA KAZINI
Na jambo jengine ni kuhusiana na
mipangilio ya Jerusalem kwa mwaka huu 2014, maana tayari ni mwezi wa pili huu
hivi sasa tunaelekea na hatujaona wala kusikia kazi yeyote mpya kutokea kwako.
Suala ambalo alinieleza kuwa wapo vyumbani wakikamilisha mapishi ya kazi mpya nyiingi
tu ambazo soon zitakuwa sokoni.
GABO AKIWA KAZINI ALIYEKUWA MAIN CHARACTER NDANI YA BADO NATAFUTA
“Kwa filamu ambzo mimi sishiriki mwaka
huu tutakuwa na filamu itakayoitwa WAGENI WANGU ambayo ameshiriki Bi
Hindu,Mhogo Mchungu,Bi Star, namzee
mwingine wa Mombasa ambayo hii itatoka recently, halafu tutakuwa na POLICE LOCK
UP ambayo atakuwepo Ben Kinyaiya,Brigit (ambaye ameigiza kama Regina) na Adam
Kuambiana, then tutakuwa na filamu nyingine inaitwaCHA USIKU ambayo wameshiriki Mayasa Mrisho,
Hemed Suleiman,Cathy Rupia, Shamsa Ford, Brigity na Baba wa Hisia “Haji Adam.
Ila kwa upande wa movie ambazo nashiriki ya kwanza kabisa itakuwa ni HUKUMU YA
NDOA YANGU ambayo nimecheza na muigizaji wa siku nyingi sana Chiki Mchoma,
Mayasa Mrisho, Shamsa Ford, Bi Mwenda, Q Chief, Brigity na Will Sanga. Ambapo
nafikiri movie hii itatoka mwezi wa tatu ama nne”
Katika malengo mazuri kabisa ya JB kwa
kutengeneza image ya kampuni yake ni pamoja na suala zima la kuwapa nafasi au kuwafungulia milango waigizaji mbalimbali
wadogo ili kuwapa nafasi na kuwa waigizaji wakubwa na waigizaji wapende kuigiza
Jerusalem
either JB yupo ama hayupo. Sasa suali langu lilikuja likiuliza kuwa je ni
kuibuavipaji au vipi maana kama ni kuibua vipaji hatujaona katika mfululizo huo
alionitajia jina ambalo ni jipya katika masikio yetu lakini pia hata katika
movie ya Bado Natafuta halikadhalika.
GABO KATIKA POUZI
“Swali zuri sana, Jerualem haibui vipaji
ila ni inaendeleza vipaji maana kuibua vipaji ni risk. Maana wapo waigizaji
waliokwisha anza kuigiza na wana vipaji, hivyo sera yetu ni kuwapa nafasi
waigizaji hao na kuwafanya wawe waigizaji wakubwa kwa kuwapa movie nyingi.”
JB AKIFURAHIA KAZI NZURI WALIYOIFANYA ZANZIBAR BAADA YA KUTWAA KITU HICHO (KOMBE0
Baada ya maongezi mengi sana na Bonge la Bwana “JB” kupitia 92.5 Hits
fm radio ikishirikiana na Www.ridhiwanshariff.blogspot.com,
kabla ya kumpa nafasi ya kuzungumza na fans wake ikanibidi na mie nimpatie
hongera yake kwa movie ya BADO NATAFUTA kwani hata mie imenivutia.
JB KATIKA POUZI YA PICHA NA JEZI YA TANZANIA
“Thanks bro, Nawaahidi kuwa movie ambazo
tumezitengeneza mwaka huu 2014 watazipenda sana maana waigizaji hawa waliocheza nimekaa
nao kwa muda mrefu tumefundishana, tumeelekezana na kila mmoja ameonesha ana
uwezo mkubwa. Hivyo nawaahidi kwamba hata movie ambazo sitashiriki watazipenda
sana kama ambazo nimeshiriki na mfano wameshaanza kuona kwa BADO NATAFUTA ni
filamu ambayo imefanya vizuri sana na hata zile ambazo nimeshiriki zingine
hazikupendwa sana kama hii ambayo sijashiriki”.
KUPITIA HAPA
HAPA Www.Michongokamili.com UTAWEZA KUSIKIA INTERVIEW YA
JACOB STEVEN NA RIDHIONE SHARIF WA ZANZIBAR
JACOB NA IRENE KAZINI